Advertisements

Wednesday, December 5, 2018

UONGOZI WA JESHI LA MAGEREZA WAKUTANA NA BALOZI MSTAAFU LT. GEN.MSTAAFU MAKAKALA LEO JIJINI DAR

 Kamishna Jenerali wa Magereza Phaustine Kasike akimkaribisha  aliyekuwa Balozi Tanzania nchini Zimbabwe Lt. Gen.Mstaafu Charles Makakala mara alipowasili  Makao Makuu ya Jeshi la Magereza Dar es Salaam leo Desemba 05, 2018 kwa ajili ya kumpongeza kwa kuteuliwa kuwa mkuu wa Jeshi hilo  na kufanya mazungumzo na uongozi wa Jeshi la Magereza.
 Aliyekuwa Balozi Tanzania nchini Zimbabwe Lt. Gen.Mstaafu Charles Makakala (wa pili kulia) akifafanua jambo alipokutana na kufanya mazungumzo  na baadhi ya viongozi wa juu wa Jeshi la Magereza leo  Desemba 05, 2018 Makao Makuu ya Jeshi la Magereza, Dar es Salaam.
 Balozi Mstaafu wa Tanzania nchini Zimbabwe Lt. Gen.Mstaafu Charles Makakala akisalimiana na Kamishna Mkuu Mstaafu wa Magereza Nicas Banzi (2002-2007) walipokutana Makao Makuu ya Jeshi la Magereza, Dar es salaam leo Desemba 05, 2018.
 Lt. Gen.Mstaafu Charles Makakala aliyewahi kuwa Balozi wa Tanzania nchini Zimbabwe (wa tatu kulia) akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya viongozi wa juu wa Jeshi la Magereza leo Makao Makuu ya Jeshi hilo. Watatu kushoto ni Kamishna Jenerali wa Magereza  Phaustine Kasike. Kulia ni Kamishna wa Sheria na Uendeshaji wa Magereza, Uwesu Ngarama na  Kamishna  wa Miundombinu ya Magereza na Uzalishaji, Tusekile Mwaisabila. Kushoto ni Kamishna wa Fedha na Mipango, Gedion Nkana na Kamishna wa Huduma za Urekebishaji, Augustino Mboje. (Picha zote na Jeshi la Magereza).

No comments: