Advertisements

Monday, March 25, 2019

KAMATI YA MIUNDOMBINU YATAKA UJENZI WA NYUMBA ZA WATUMISHI MZANI WA DAKAWA

 Naibu Waziri wa Ujenzi, Elias Kwandikwa, akifafanua jambo kwa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu kuhusu maendeleo  ya ujenzi wa kituo cha Mizani kinachojengwa Dakawa Mkoani Morogoro, wakati kamati hiyo ilipokagua mzani huo. Wa nne kushoto ni Mwenyekiti wa Kamati hiyo Suleiman Kakoso.
 Mafundi wa Kampuni ya Group Six International wakiendelea na ufungaji wa Kamera katika mzani mpya unaojengwa eneo la Dakawa mkoani Morogoro.
 Muonekano wa jengo la mzani mpya unaojengwa Dakawa Mkoani Morogoro. Mradi huo umekamilika kwa asilimia 98.
Mhandisi Mshauri Kasmir Mustapha (kulia), akitoa taarifa kwa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu kuhusu maendeleo  ya ujenzi wa kituo cha Mizani kinachojengwa Dakawa Mkoani Morogoro, wakati kamati hiyo ilipokagua mzani huo.

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu imeishauri Serikali kupitia Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya Ujenzi), kujenga nyumba za watumishi kwenye mzani mpya unaojengwa Dakawa Mkoani Morogoro ili kuwapunguzia adha wafanyakazi watakaokuwa wakifanya kazi kituoni hapo.
Akizungumza mara baada ya kukagua mradi huo, Mwenyekiti wa Kamati hiyo Mhe. Moshi Sulemani Kakoso ameipongeza Wizara na kuhakikisha kuwa pamoja na kujengewa nyumba hizo, pia Wizara iwasimamie watumishi wa mzani vizuri ili kuepuka vitendo vya rushwa.
"Serikali imetumia fedha nyingi kujenga mzani huu, nawapongeza sana lakini sasa ni muhimu watumishi wa mzani huu wakasimamiwa vyema ili kuepuka vitendo vya rushwa vinavyofanywa na watumishi wasio waaminifu" amesema Mwenyekiti. Kakoso.
Mwenyekiti Kakoso, ametoa wito kwa wafanyabiashara wote nchini kuhakikisha wanazingatia sheria za mizani kwa kupakia mizigo isiyozidi kiwango ili kulinda miundombinu ya barabara nchini.
Kwa upande wake Naibu Waziri wa Ujenzi, Elias Kwandikwa, ameihakikishia Kamati hiyo kuwa Serikali imejipanga kuhakikisha changamoto zote zilizowasilishwa zinatatuliwa mapema ili kuongeza ufanisi.
Naibu Waziri huyo ameieleza kamati hiyo kuwa ujenzi wa mzani huo unatarajiwa kukamilika mwishoni mwa mwezi Machi mwaka huu kwa gharama ya zaidi ya shilingi Bilioni 14.
Naye Mkuu wa Kitengo cha Usalama na Mazingira kutoka Sekta ya Ujenzi Mhandisi Julius Chambo, amesema ujenzi wa mzani huu unatokana na mzani wa Kihonda kuzidiwa na msongamano wa magari kwa kuwa ni wa upande mmoja.
Ameeleza kuwa ukamilikaji wa mzani huu utasaidia kuokoa muda kwa wasafirishaji na kuondosha msongamano uiopo sasa katika mzani wa Kihonda kwani mzania huu utapima tu yale magari yanayoonekana yamezidi uzito tu.

No comments: