Advertisements

Thursday, March 14, 2019

Serikali ya Zanzibar kujenga hospitali mithili ya Mloganzila

  Katibu Mkuu Wizara ya Afya Zanzibar Asha Ali Abdulla (aliyevaa mtandio wa bluu) akizungumza na viongozi wa Hospitali ya Taifa Muhimbili Mloganzila na Upanga mara baada ya kuwasili Mloganzila kwa ziara maalum ya kujifunza. Kushoto kwake ni Mkurugenzi Mtendaji wa Muhimbili Prof. Lawrence Museru.
 Mhandisi wa mitambo katika Hospitali ya Mloganzila Bw. Akaniwa Msengi (kushoto) akielezea jinsi mitambo ya hewa safi inavyofanya kazi.
 Watendaji wa Wizara ya Afya Zanzibar wakiendelea kupata maelezo ya kina juu ya mitambo mbalimbali inavyofanya kazi hospitalini hapo.
  Mkuu wa Idara ya Magonjwa ya ndani na wagonjwa wa nje Dkt. Rose Minja (aliyevaa koti jeupe) akitoa maelezo ya huduma zinazofanyika katika idara hiyo.
 Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya Zanzibar Asha Ali Abdulla (katikati) pamoja na Mhandisi Cosmas Masolwa wakipatiwa maelezo na Msimamizi wa kitengo cha kusafisha damu kwa magonjwa ya figo Bw. Emanuel Mlay (kushoto) kuhusu huduma ya kusafisha damu inavyotolewa hospitalini hapo.
 Kaimu Meneja wa maabara Mloganzila Esuvat Moses (kulia) akifafanua namna maabara inavyofanya kazi, vipimo vinavyotolewa pamoja na aina ya mashine zilizopo katika maabara hiyo.
 Daktari Bingwa wa magonjwa ya dharura katika Hospitali ya Mloganzila Henry Sawe (kushoto) akiwaelezea watendaji wa Wizara ya Afya Zanzibar jinsi huduma za dharura zinavyofanyika hospitalini hapo.
Katibu Mkuu Wizara ya Afya Zanzibar Asha Ali Abdulla (wa nne kutoka kushoto kwa walioketi) akiwa katika picha ya pamoja na viongozi wa wizara hiyo na wa Muhimbili, kulia kwakwe ni Mkurugenzi Mtendaji wa MNH Prof. Lawrence Museru akifuatiwa na Kaimu Naibu Mkurugenzi Mtendaji wa Mloganzila Dkt. Julieth Magandi.

No comments: