Advertisements

Thursday, April 25, 2019

WIZARA YA AFYA, SHIRIKA LA WHO WATOA ELIMU UELEWA WA CHANJO KWA WANAHABARI DAR ES SALAAM


Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Kinga na Meneja wa Mpango wa Taifa Chanjo, Dk. Dafrossa  Lyimo akizungumza kwenye hitimisho la semina maalum kwa waandishi wa habari mbalimbali,juu ya uelewa wa Chanjo hapa nchini. Tukio lililofanyika mapema leo Jijini Dar es Salaam.


NA Andrew Chale.

WIZARA  ya  Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia wazee na Watoto kwa kushirikiana na Wadau wengine wakiwemo Shirika la Afya Duniani (WHO) mapema leo wameendesha  semina maalum  kwa Waandishi wa Habari juu ya uelewa wa Chanjo zinazotolewa hapa nchini, tokea  kuanzishwa kwake mwaka 1975.

Tanzania walianza kutoa Chanjo aina tano (5)  pekee, lakini mpaka kufikia sasa  imevuka hatua  na kufikia kutoka aina 15 za Chanjo. Wizara ya Afya katika mpango wake ,  inasisitiza wazazi kuhakikisha watoto wao wanapata chanjo zote zinazotakiwa kwa wakati  ili waweze kuepukana na magonjwa mbalimbali.

Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Kinga na Meneja wa Mpango wa Taifa Chanjo, Dk. Dafrossa  Lyimo amesema kuwa  chanjo ni bure na inapatikana kila Zahanati, vituo vya afya na maeno husika hivyo wahitajika wa Chanjo wanatakiwa kupelekwa nakupatiwa wakiwemo watoto ambao ndio wenye uhitaji mkubwa .

“Chanjo ni bure. Lakini kuna watu wamekimbia chanjo, ndio maana tunawaomba wanahabari mtusaidie kutoa elimu ili watu wakapate chanjo.  Na tungependa kila baada ya miezi mitatu tukutane na nyie Wanahabari. Tunawaomba mtufikishie hizi habari kwa Club zenu za Wanahabari ili taarifa za Chanjo zienee kote” alisema Dk. Dafrossa Lyimo akisisitiza kwa Wanahabari.

Akielezea ugonjwa wa Surua na  Rubella, alifafanua kuwa, ugonjwa huo unafanana lakini kwa Rubella wamama wanaoshika ujauzito, madhara yake ni kwa mototo atakayezaliwa kuwa na shida kwenye ini, ana tundu kwenye moyo, figo na maeneo mengine.

“Surua na Rubella dalili zake zinafanana kwa karibu sana. Unaweza kuja na dalili za surua, lakini mpaka ufanye vipimo kwa ukaribu sana ndio unakuta ni Rubella lakini chanjo zake ni moja lakini ni magonjwa mawili tofauti yaani surua na Rubella.” Alieleza Dk. Dafrossa Lyimo wakati wa kufafanua ugonjwa wa Surua na Rubella.

Akielezea ugonjwa wa Polio, amebainisha kuwa, kwenye ugonjwa mmoja anaweza kuambukiza watu zaidi ya 2,00   ndio maana wanahamasisha watu wapate chanjo  ilikuepuka matitizo  kwani tatizo la ugonjwa huo upotez pia nguvu kazi ya Taifa.

Adiha, Dk.Dafrossa Lyimo amewataka Waandishi wa habari kuzingatia  na kuacha mazoea, Chanjo haipo kwenye kidonge, bali chanjo ipo kwenye mfumo wa sindano ama tone (maji ) na mfumo huo mpaka sasa haujabadilishwa.

“Mtu akikuletea kidonge akikuambia chanjo  hiyo sio chanjo,  hiyo ni kinga tiba na unaweza kunywa muda wowote mfano dawa ya kinga ya minyoo ama mabusha hiyo haina ratiba kila mwaka unakunywa, ya kwetu Chanjo ina muda maalum.” Alieleza Dk. Dafrossa Lyimo.

Pia amewataka Jamii kuzingatia kumaliza dozi za kinga kwa wakati hii ni kwa kufuata ratiba watakazowekewa na watalaam.

 Dk. Dafrossa Lyimo amebainisha kuwa, Chanjo ni haki ya kila mototo, hivyo wanatakiwa wapeleke  kwenye vituo vya kutolea huduma za afya akapate chanjo.

Imeelezwa kuwa, chanjo siyo tu zinaokoa maisha, bali uboresha maisha  pia  huku kwa mwaka huu kauli mbiu ikiwa:  “Chanjo ni kinga, kwa pamoja tuwakinge” .

Nae Mwakilishi wa Shirika la Afya Duniani (WHO), Mtalaam wa Chanjo, Dk. William Mwengee amebainisha kuwa, Tanzania imepiga hatua katika masuala ya chanjo kwa kuweza kuhakikisha chanjo inafika kwa wakati karibu maeneo yote licha ya changamoto ya usafiri ama wa kifedha inayotokea baadhi ya maeno ya Nchi kutokana na hali halisi ya wakati huo.

Dk Mwengee ameongeza kuwa, Tanzania ni moja kati ya nchi ambazo zinachukua hatua ya kuwa na chanjo ili kuhakikisha kuwa maradhi yanayozuilika hayaendelei kuwa tatizo tena na kuhakikisha kwamba watoto wote wanaozaliwa hospitalini au nje ya hospitali wanapata huduma zote za chanjo kama ilivyo pangwa ambapo imeweza kufanikiwa kwa kiwango kikubwa.

“Magonjwa yanayodhuilika ya chanjo, yanaua, tena yanaua kwa kiwango kikubwa sana, hivyo tunao wajibu wa kutumia kalamu zetu kupaza sauti juu ya watu wakapate chanjo” alieleza Dk. Mwangee.

Kila mwezi wa Nne (Aprili) ni wiki ya Chanjo Barani Afrika, ambapo  jamii imetakiwa kuhakikisha motto anakamilisha chanjo. Ambapo chanjo hiyo uwakinga watoto dhidi ya  ugonjwa wa Polio, Surua, Rubella, Kuhara, donda koo, Kifaduro, Pepopunda, homa ya ini, kifua kikuu, Homa ya Uti wa mgongo, Nimonia na mengine mengi.

Watalaam hao wameweka wazi kuwa, Mtoto asiyepata Chanjo, ni hatari kwa maisha yake na jamii inayomzunguka sababu anaweza kuambukizwa magonjwa na kuambukiza wengine.









Mwakilishi wa Shirika la Afya Duniani (WHO), Mtalaam wa Chanjo, Dk. William Mwengee akizungumza katika semina hiyo kwa wanahabari











Mwanahabari James Kandoya wa The Guardian, akiuliza swali kuhusiana na masuala ya Chanjo



Wanahabri wakijadili mada kwenye semina hiyo




Mwakilishi wa Shirika la Afya Duniani (WHO), Mtalaam wa Chanjo, Dk. William Mwengee akiteta na mwandishi wa habari wa THE CITIZEN, John NK.

Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Kinga na Meneja wa Mpango wa Taifa Chanjo, Dk. Dafrossa  Lyimo akizungumza kwenye hitimisho la semina maalum kwa waandishi wa habari mbalimbali,juu ya uelewa wa Chanjo hapa nchini. Tukio lililofanyika mapema leo Jijini Dar es Salaam.



Mwakilishi wa Shirika la Afya Duniani (WHO), Mtalaam wa Chanjo, Dk. William Mwengee akizungumza katika semina hiyo kwa wanahabari

   
Mtaalamu wa Chanjo kutoka Wizara ya Afya, Lotalis Gadau akizungumza katika semina hiyo

No comments: