Advertisements

Wednesday, July 17, 2019

Prof. Kabudi azungumza na Mabalozi wastaafu wa Tanzani

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb.) amekutana na kufanya mazungumzo na Mabalozi wastaafu walioiwakilisha Tanzania katika nchi mbalimbali duniani kwa nia ya kupata ushauri na maoni yao kuhusu maandalizi ya Mkutano wa 39 wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC). Mkutano huo umefanyika katika ukumbi wa kimataifa wa Julius Nyerere uliopo jijini Dar es Salaam. Katika mkutano huo Prof. Palamagamba John Kabudi ameongozana na Naibu Waziri wa Wizara ya Mambo ya Nje Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro (Mb.), Katibu Mkuu Dkt. Faraji Kasidi Mnyepe (wa kwanza kushoto) na Naibu Katibu Mkuu Balozi Ramadhani Muombwa Mwinyi (wa kwanza kulia). 
Juu na Chini ni sehemu ya Mabalozi wastaafu walioiwakilisha Tanzania katika nchi mbalimbali duniani wakimsikiliza Mhe. Prof. Palamagamba John Kabudi (hayupo pichani). 
Sehemu ya watumishi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki wakimsikiliza Prof. Palamagamba John Kabudi (hayupo pichani) 
Mkutano ukiendelea
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb.), Naibu Waziri Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro (Mb.), Katibu Mkuu Dkt. Faraji Kasidi Mnyepe, Naibu Katibu Mkuu Balozi Ramadhani Mwinyi wakiwa katika picha ya pamoja na Mabalozi wastaafu walioiwakilisha Tanzania katika nchi mbalimbali duniani 

No comments: