Advertisements

Thursday, July 18, 2019

UJENZI KIVUKO CHA KAYENZE KWENDA KISIWA CHA BEZI MWANZA KUKAMILIKA NOVEMBA 2019

Mkurugenzi wa Songoro Marine Ltd Meja Songoro akimuonesha Mbunge wa Jimbo la Ilemela na Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Angeline Mabula (wa kwanza kushoto) maendeleo ya ujenzi wa Kivuko cha Kayenze kwenda Kisiwa cha Bezi mkoani Mwanza wakati wa ziara yake ya kukagua kivuko hicho kinachotarajiwa kukamilika Novemba 2019.
Mbunge wa Jimbo la Ilemela ambaye pia ni Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Angeline Mabula akishuka kutoka katika kivuko cha Kayenze kwenda Kisiwa cha Bezi mkoani Mwanza wakati alipofanya ukaguzi wa kivuko hicho kinachotarajiwa kukamilika Novemba 2019.
Mkurugenzi wa Songoro Marine Ltd Meja Songoro akimuonesha Mbunge wa Jimbo la Ilemela na Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Angeline Mabula (wa kwanza kushoto) maendeleo ya ujenzi wa Kivuko cha Kayenze kwenda Kisiwa cha Bezi mkoani Mwanza wakati wa ziara yake ya kukagua kivuko hicho kinachotarajiwa kukamilikaNovemba 2019.
Mbunge wa Jimbo la Ilemela ambaye pia ni Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Angeline Mabula akizungumza ndani ya kivuko cha Kayenze kwenda Kisiwa cha Bezi mkoani Mwanza na ujumbe alioambatana nao wakati alipofanya ukaguzi wa kivuko hicho kinachotarajiwa kukamilika Novemba 2019.
Mbunge wa Jimbo la Ilemela ambaye pia ni Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Angeline Mabula akiangalia kivuko cha Kayenze kwenda Kisiwa cha Bezi mkoani Mwanza wakati alipofanya ukaguzi wa kivuko hicho kinachotarajiwa kukamilika Novemba 2019.
Mbunge wa Jimbo la Ilemela ambaye pia ni Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Angeline Mabula akikagua maendeleo ya ujenzi wa kivuko cha Kayenze kwenda Kisiwa cha Bezi mkoani Mwanza wakati alipofanya ukaguzi wa kivuko hicho kinachotarajiwa kukamilika Novemba 2019.

Na Munir Shemweta, WANMM MWANZA

Ujenzi wa kivuko cha Kayenze kwenda Kisiwa cha Bezi mkoani Mwanza unaogharibu kiasi cha bilioni 2.7 unatarajiwa kukamilika Novemba mwaka 2019.

Hayo yamebainika juzi wakati Mbunge wa jimbo la Ilemela mkoani Mwanza ambaye pia ni Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Angeline Mabula alipotembelea kivuko hicho kuangalia maendeleo ya ujenzi ikiwa ni utekelezaji wa ahadi aliyoitoa kwa wananchi wa jimbo lake wakati wa uchaguzi mkuu uliofanyika 2015.

Kwa mujibu wa Dkt Mabula, kivuko cha Kayenze kwenda Kisiwa cha Bezi chenye uwezo wa kubeba abiria 250, magari 10 na ukubwa wa tani 10 kitaondoa kero ya muda mrefu waliyokuwa wakiipata wananchi wa Kayenze na Bezi katika suala la huduma ya usafiri wa majini.

‘’Wananchi wa Kisiwa cha Bezi na Kayenze Mwaloni wamekuwa na shida ya usafiri majini kwa muda mrefu na mimi niliahidi kuwapatia kivuko wakati wa uchaguzi mwaka 2015 na ombi langu la kujenga kivuko hicho lilipokelewa vyema na serikali toka mwaka 2016 kwa ahadi ya kujenga kivuko hicho’’ Alisema Dkt Mabula.

Mbunge huyo wa Jimbo la Ilemela alisema, kuchelewa kukamilika mapema kivuko hicho kulitokana na changamoto kadhaa na mojawapo ni kukwama kwa vifaa bandarini kulikosababishwa na msamaha wa ushuru ambapo hata hivyo, Dkt. Mabula aliahidi kushughulikia suala hilo na kufafanua kuwa Oktoba mwaka 2019 kivuko hicho kitafanyiwa majaribio rasmi kabla ya kukabidhiwa mwezi mmoja baadaye kwa ajili yua kuanza kazi rasmi.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Kampuni inayotengeneza kivuko hicho ya Songoro Marine Ltd Meja Songoro alisema ujenzi wa kivuko higho ulioanza Januari 2019 uko katika hatua za mwisho za ukamilishaji ambapo sasa kampuni yake inakamilisha kufunga mifumo ya maji, umeme, zimamoto , kufunga ingini na vifaa vya kuendeshea kivuko hicho.

Kwa mujibu wa Songoro, kampuni hiyo ya Songoro Marine Ltd ni mahiri katika kutengeneza vivuko na kutolea mfano wa vivuko vya Mv Mwanza, Kazi pamoja na kile cha Geita kuwa ni vivuko vilivyofanyiwa kazi na kampuni yake na kufafanua kuwa hivi sasa kampuni hiyo imepata kazi za vivuko katika nchi jirani za Kenya na Uaganda

No comments: