Spika wa Bunge, Mhe. Job Ndugai akizungumza na waandishi wa habari katika kikao kilichofanyika nyumbani kwake uzunguni Jijini Dodoma Mei 18, 2020. Mhe. Ndugai ametangaza mabadiliko ya ratiba ya shughuli za Bunge la 11 ambapo bajeti kuu ya serikali itasomwa tarehe 11 Juni 2020 na shughuli za Bunge zitamalizika Juni 19, 2020 ambapo Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli atatoa hotuba ya mwisho ya kulivunja bunge.
Spika wa Bunge, Mhe. Job Ndugai akiongoza kikao cha kamati ya uongozi kilichokaa ili kupokea Mapendekezo ya Mabadiliko ya Ratiba ya Mkutano wa 19 wa Bunge leo nyumbani kwake uzunguni Jijini Dodoma Mei 18, 2020.
No comments:
Post a Comment