Advertisements

Thursday, October 29, 2020

MHE.LISSU APIGA KURA KWENYE JIMBO LA IKUNGI MKOANI SINGIDA


NA EMMANUEL MBATILO

Mgombea Urais kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA Mhe.Tundu Lissu ameupongeza uongozi katika kituo alichopigia Kura pamoja na maeneo mengi ya Mkoa wa Singida zoezi hilo kuripotiwa kwenda vizuri.

“Zoezi limekwenda vizuri nafikiri kwa njinsi nilivyoona utaratibu uko vizuri, Wasimamizi wa kituo,waongozaji,mawakala kuna kila dalili ya kuonesha kwamba kwenye kituo hiki mambo yamekwenda vizuri lakini hapa jimboni kwangu kwa watu wangu sijapata taarifa yoyote kwamba mambo hayajaenda sawa sawa”. Amesema Mhe.Lissu.

No comments: