Advertisements

Saturday, January 16, 2021

Gaga na Lopez kutumbuiza katika sherehe za kuapishwa kwa Biden

Washington, Marekani, MTANZANIA

Lady Gaga na Jennifer Lopez wanatarajia kutumbuiza kwenye sherehe ya kuapishwa kwa Joe Biden, ambaye alichaguliwa kuwa rais wa Marekani itakayofanyika mnamo Januari 20.

Jennifer Lopez atatumbuiza kwenye sherehe hiyo ambapo Lady Gaga ataimba wimbo wa taifa wa Marekani.

Sherehe ya kiapo itafanyika na ushiriki wa idadi ndogo ya watu baada ya janga la corona na uvamizi wa Bunge la Marekani mnamo Januari 6.

Jon Bon Jovi, Justin Timberlake na Demi Lovato pia watatumbuiza kwenye sherehe ya uzinduzi ambapo muigizaji maarufu wa Marekani Tom Hanks atakuwa mtangazaji.

Siku ya sherehe ya kula kiapo, walinzi elfu 20 wa kitaifa watahudumu katika mji mkuu, Washington, ambapo hatua za usalama zimepandishwa kwa kiwango cha juu zaidi.

No comments: