Thursday, January 28, 2021

RAIS DKT MAGUFULI AFUNGUA MAJENGO MAPYA NA UPANUZI WA HUDUMA KITUO CHA AFYA CHA MASUMBWE WILAYA YA MBOGWE MKOA WA GEITA

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwasili ili kufungua majengo mapya na upanuzi wa huduma katika Kituo cha Afya cha Masumbwe Wilaya ya Mbogwe Mkoa wa Geita akiongozana na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Dorothy Gwajima na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais
TAMISEMI Mhe. Selemani Jaffo leo Jjumatano Januari 27, 2021
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na baadhi ya wagonjwa waliolazwa katika Kituo cha Afya cha Masumbwe wilayani Mbogwe leo Jjumatano Januari 27, 202
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akizindua majengo mapya na upanuzi wa huduma Kituo cha Afya cha Masumbwe Wilaya ya Mbogwe Mkoa wa Geita akiwa na Waziri wa Afya Dkt. Doroth Gwajima na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI Mhe. Selemani Jaffo na viongozi wengine leo Jjumatano Januari 27, 2021.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akitoka kutembelea sehemu mbalimbali za Kituo cha Afya cha Masumbwe wilayani Mbogwe wakati wa sherehe za ufunguzi wa Majengo Mapya na Upanuzi wa Huduma katika kituo hicho leo Jjumatano Januari 27, 2021.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na wananchi wa Masumbwe mara baada ya kufungua Majengo mapya ya Kituo cha Afya cha Masumbwe Mbogwe mkoani Geita leo tarehe 27 Januari 2021.
Wananchi wa Masumbwe wakishangilia wakati walipokuwa wakisikiliza hotuba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli mara baada ya kufungua Majengo mapya ya Kituo cha Afya cha Masumbwe Mbogwe mkoani Geita.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwa ameshika picha ya kuchora aliyozawadiwa na kijana Emanuel Nande mkazi wa Mbogwe (kulia) mara baada ya kuwahutubia wananchi wa Mbogwe mkoani Geita

PICHA NA IKULU

No comments: