Saturday, September 28, 2024

MAHAFALI YA 46 YA BODI YA NBAA YANG'ARA


Wahitimu wa Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu (NBAA) wakiwa kwenye maadamano ya kitaaluma wakati wa mahafali ya 46 ya Bodi hiyo yaliyofanyika katika hoteli ya APC Bunju, Dar es Salaam.
Naibu Waziri wa Fedha Mhe. Hamad Hassan Chande akipokea maadamano ya kitaaluma pamoja na viongozi wa Bodi pamoja na wajumbe wa Bodi hiyo wakati wa mahafali ya 45 ya Bodi hiyo 


Naibu Waziri wa Fedha Mhe. Hamad Hassan Chande akisoma hotuba yake kwenye mahafali ya 46 ya Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu  Tanzania (NBAA).
Mwenyekiti wa Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu Tanzania (NBAA), CPA. Prof. Sylvia S. Temu akizungumza kuhusu namna Bodi hiyo ilivyofanikisha kuongeza idadi ya wahitimu kwa mwaka huu wa 2024 pamoja na kuelezea mafanikio mbalimbali ambayo Bodi imeyapata toka kuanzishwa kwake.
Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu Tanzania (NBAA), CPA Pius A. Maneno akitoa ufafanuzi namna Bodi hiyo inavyofanya kazi kwa  Naibu Waziri wa Fedha Mhe. Hamad Hassan Chande.
Baadhi ya Wahitimu pamoja na wageni waalikwa wakifuatilia hotuba ya mgeni rasmi Naibu Waziri wa Fedha Mhe. Hamad Hassan Chande kwenye mahafali ya 46 ya Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu Tanzania (NBAA).
Wahitimu wa ngazi ya CPA wakisoma viapo vyao wakati wa mahafali ya 46 ya Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu Tanzania (NBAA) 
Naibu Waziri wa Fedha Mhe. Hamad Hassan Chande akiwatunuku wahitimu kwenye mahafali ya 46 ya Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu  Tanzania (NBAA).
Wahitimu wakishangilia mara baada ya kutunukiwa CPA wakati wa mahafali ya 46 ya Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu  Tanzania (NBAA)
Naibu Waziri wa Fedha Mhe. Hamad Hassan Chande akitoa vyeti kwa baadhi ya wahitimu waliofanya vizuri kwenye mitihani ya Bodi wakati wa mahafali ya 46 ya Bodi hiyo.
Naibu Waziri wa Fedha Mhe. Hamad Hassan Chande akiwa kwenye picha ya pamoja na baadhi ya wahitimu wa Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu (NBAA) kwenye ngazi za ATEC, CPA, na IPSAS wakati wa mahafali ya 46 ya Bodi hiyo yaliyofanyika katika hoteli ya APC Bunju, Dar es Salaam.
Naibu Waziri wa Fedha Mhe. Hamad Hassan Chande akiwa kwenye picha ya pamoja na baadhi ya wafanyakazi wa Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu (NBAA) wakati wa mahafali ya 46 ya Bodi hiyo.

No comments: