Monday, July 16, 2012

MANJI MWENYEKITI MPYA YANGA

HATIMAYE wanachama wa Yanga kwa moyo mmoja usiku wa kuamkia leo walimchagua mfadhili wao wa zamani, Yusuf Manji kuwa mwenyekiti wa timu hiyo, lakini majira ya saa nane usiku kabla hajatangazwa zilizuka vurugu kubwa.
Yanga jana ilifanya uchaguzi wa kujaza nafasi kadhaa ambazo ziliachwa wazi baada ya mwenyekiti wa zamani wa timu hiyo, Llyod Nchunga, makamu mwenyekiti, Davies Mosha na wajumbe kadhaa kujiuzulu kutokana na mwenendo mbaya wa timu hiyo.
Katika uchaguzi huo uliofanyika kwenye Ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar, zaidi ya wanachama 2,000 walipiga kura, huku amani ikitawala kuanzia hatua za awali, lakini hali mbaya ilizuka usiku majira ya saa nane baada ya walinzi kujisahau na kufungua geti wakifikiri kuwa kura zimemalizika kuhesabiwa, ndipo mamia ya wanachama waliokuwa nje ya ukumbi huo kuingia ndani kwa kasi.
Hata hivyo, wasimamizi waliwataka wanachama hao kutoka nje kwanza kwani kura za mwenyenyekiti zilikuwa bado hazijahesabiwa, hali iliyozua zogo na kejeli za hapa na pale.

No comments: