Wednesday, October 30, 2013

WANADMV WAMFARIJI MAYOR MLIMA


 WanaDMV waliofika nyumbani kwa Mayor Mlima 9205 New Hampshire Ave Apt 207, Silver Spring, MD 20903 Jumanne Oct 29, 2013 kumfariji baada ya siku ya Jumampili Oct 27, 2013 kufikwa na msiba wa mdogo wake Luteni Rajabu Ahmed Mlima uliotokea DRC baada ya marehemu kupigwa risasi wakati jeshi la kulinda amani walipokuwa wakijaribu kukinga raia wasidhurike na mapigano kati ya majeshi ya serikali na kikundi cha M23 katika uwanja kwenye milima ya Gavana.
 WanaDMV wakiwa nyumbani kwa Mayor Mlima.
 Bwn. Deo Ruta katika picha
 Kushoto ni Colonel Adolph Mutta, Mwambata wa Jeshi wa Ubalozi wa Tanzania nchini Marekani na Canada akijumuika na WanaDMV nyumbani kwa Mayor Mlima
 Juu na chini ni WanaDMV wakimfariji Mayor Mlima nyumbani kwake Silver Spring, Maryland.

No comments: