Wednesday, October 30, 2013

Waziri ahamasisha uwekezaji katika sekta ya kilimo Tanzania


Urban Pulse Creative Media, Ubalozi wa Tanzania wakishirikiana na Freddy Macha wanakuletea ziara ya Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika, Mhandisi Christopher
Chiza alipokutana na wawekezaji jijini London tarehe 21 Octoba 2013.

Mkutano huu ulifanyika katika ukumbi wa Reform Club mtaa wa Pall Mall, London,
na kuhusisha wafanyabiashara wenye shughuli za kilimo Tanzania, makampuni
makubwa yanayojishughulisha bara Asia, Afrika na Uingereza, mathalan duka
maarufu la Sainsburys.

No comments: