ANGALIA LIVE NEWS

Wednesday, June 18, 2014

HASIRA HASARA: MWANAMKE AJINYONGA KWA KHANGA KWA HASIRA ZA KUFIWA NA MWANAE



Na Walter Mguluchuma
Mpanda Katavi
Mwanamke mmoja aliyefahamika kwa jina la Mwashi  Ngehu(38) Mkazi wa Kijiji cha Chamalendi  Tarafa ya   Mpimbwe Wilaya ya Mlele  Mkoa wa Katavi amefariki Dunia   kwa  kujinyonga   kwa kutumia khanga  baada ya kupatwa na hasira ya kufiwa na mtpto wake wa Kike
Kwa mujibu wa Kamanda wa jeshi la Polisi wa Mkoa wa Katavi Dhahiri Kidavashari  tukio hilo lilitokea hapo jana majira ya saa kumi na moja alifajiri Kijijni hapo
Katika tukio hilo ni kwamba marehemu  marehemu  alikuwa akimuuguza mwanae wa kike kwa muda wa miezi miwili  ambae alikuwa  ni mtoto pekee wa marehe huyo
Alisema ndipo hapo juzi mwae huyo alifariki   dunia na kuzikwa kijijini hapo na muda wote wa msiba  marehemu alikuwa akilia kwa uchungu  kufiwa na mwanae huyo wa pekee
Kidavashari alieleza  marehemu  alikuwa akiwaeleza waombolezaji waliofika kufariji msibani  kuwa   amepatwa na uchungu sana kufiwa na mtoto wake  ambae alimzaa  kwa shida  sana kwani  waliishi na mume wake kwa muda mrefu bila kujaliwa kupata mtoto
Alisema marehemu alikuwa akiwaeleza waombolezaji kuwa haoni faida ya kuishi tena Dunia  bila kuwa na mtoto yoyote yule

Alieleza ndipo hapo juzi majira ya usiku  wakati alipokuwa amelala ndani ya nyumba yake  alipotoka nje  na kuwaaga ndugu zake waliokuwapo msibani hapo kuwa anatoka nje kwenda kujisaidia
Alisema marehemu  hakurejea tena ndani ya nyumba hadi hapo  juzi  majira ya saa kumi na moja mwili wake ulipokutwa  ukiwa unang’inia juu ya mti huku akiwa  amejinyonga hadi kufa kwa kutumia khanga yake
Mwili wa marehemu umeisha fanyiwa uchunguzi wa Kidakitari na wamekabidhiwa ndugu zake kwa ajiri ya mazishi ambayo  yalifanyika hapo jana kijini hapo

No comments: