Jeshi la polisi na JWTZ wafanikiwa kuharibu bomu lililotelekezwa Mtwara.
Jeshi
la polisi mkoani Mtwara kwa kushirikiana na jeshi la wananchi wa
Tanzania wamefanikiwa kuharibu bomu lililokuwa limetelekezwa katika
kijiji cha Mdui kata ya Mbawala wilaya ya Mtwara vijijini baada ya
kuonekana likichezewa na watoto.
jeshi la polisi mkoani Mtwara kwa kushirikiana na
jeshi la wananchi wa Tanzania wamefanikiwa kuharibu mlipuko wa bomu
katika kijiji cha Mdui kata ya Mbawala wilaya ya Mtwara vijijini baada
ya kuonekana likichezewa na watoto.
Akizungumza na ITV kaimu kamanda wa
polisi mkoa wa Mtwara Maisha Maganga amesema taarifa hizo wamezipata kutoka kwa raia wema baada ya kuonekana likiwa eneo la makaburi.
polisi mkoa wa Mtwara Maisha Maganga amesema taarifa hizo wamezipata kutoka kwa raia wema baada ya kuonekana likiwa eneo la makaburi.
Amesema baada ya kupata taarifa juu ya bomu hilo
lenye kilo nne jeshi hilo lilichukua hatua za haraka ikiwa ni pamoja na
kuomba kikosi maalum cha kutegua mabomu kutoka jeshi la wananchi wa
Tanzania.
Amesema bomu hilo linaonyesha ni la siku nyingi mahali hapo na liliachwa enzi za vita ya Msumbiji.
1 comment:
mbona huko mtwara liliteguliwa zanzibar liki uwa mtu?
Post a Comment