Advertisements

Wednesday, August 9, 2017

KANISA LA KIINJILI LA KILUTHERI TANZANIA (KKKT) MTAA WA MWAPEMWA USHARIKA WA MTONI WAFANYA HARAMBEE YA KUCHANGIA UJENZI WA KANISA

 Mratibu wa Idara ya huduma za jamii wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT)  Jimbo la Kusini Mchungaji  Andrew King’omela akizungumza na Mwinjilisti kiongozi wa Mtaa Mwapemba Usharika wa Mtoni Nicolas Mtali wakati wa harambee ya kuchangia ujenzi wa kanisa la Mtaa huo iliyofanyika hivi karibuni. Zaidi ya milioni 17 zilipatikana katika harembee hiyo ambayo ilikadiriwa kukusanya kiasi cha milioni 50.
 Mratibu wa Idara ya huduma za jamii wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT)  Jimbo la Kusini Mchungaji  Andrew King’omela (kushoto) akizungumza na Mchungaji wa Usharika wa Mtoni Moses Sozigwa (kulia) ambaye ni mlezi wa Mtaa wa Mwapemba wakati wa harambee ya ujenzi wa kanisa la Mtaa huo.
  Kwaya ya Uinjilisti ya Mtaa wa Kemete usharika wa Kijitonyama ikiimba wakati wa harembee ya kuchangia ujenzi  wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Jimbo la Kusini  Mtaa wa Mwapemba Usharika wa Mtoni iliyofanyika hivi karibuni. Zaidi ya milioni 17 zilipatikana katika harembee hiyo ambayo ilikadiriwa kukusanya kiasi cha milioni 50.
 Waumini wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Jimbo la Kusini  Mtaa wa Mwapemba Usharika wa Mtoni pamoja na wageni mbalimbali waliohudhuria harambee ya kuchangia ujenzi wa kanisa hilo wakimsikiliza Mratibu wa Idara ya huduma za jamii  Mchungaji  Andrew King’omela akihubiri.
 Viongozi wa Kwaya ya Uinjilisti ya Mtaa wa Kemete usharika wa Kijitonyama wakinadi kanga ambayo iliuzwa shilingi 67,000/= wakati wa harembee ya kuchangia ujenzi  wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Jimbo la Kusini  Mtaa wa Mwapemba Usharika wa Mtoni iliyofanyika hivi karibuni. Zaidi ya milioni 17 zilipatikana katika harembee hiyo ambayo ilikadiriwa kukusanya kiasi cha milioni 50.
 Wachungaji pamoja na wazee wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Jimbo la Kusini  Mtaa wa Mwapemba Usharika wa Mtoni wakiingia katika ibada maalum ya harambee ya kuchangia ujenzi wa kanisa iliyofanyika hivi karibuni. Zaidi ya milioni 17 zilipatikana katika harembee hiyo ambayo ilikadiriwa kukusanya kiasi cha milioni 50.
 Wajumbe wa kamati ya Ujenzi wa  Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Jimbo la Kusini  Mtaa wa Mwapemba Usharika wa Mtoni wakihesabu fedha zilizotolewa na wadau mbalimbali waliohudhuria harambee ya kuchangia ujenzi wa kanisa hilo iliyofanyika hivi karibuni. Zaidi ya milioni 17 zilipatikana katika harembee hiyo ambayo ilikadiriwa kukusanya kiasi cha milioni 50.
 Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Jimbo la Kusini  Mtaa wa Mwapemba Usharika wa Mtoni lenye uwezo wa kuchukuwa waumini 400  na vyumba vya ofisi vitano kama linavyoonekana katika picha.
Picha na Anna Nkinda

No comments: