Advertisements

Sunday, August 13, 2017

RAIS MSTAAFU AWAMU YA PILI ALI HASSAN MWINYI AWAASA MADEREVA KUZINGATIA SHERIA ZA BARABARANI ILI KUEPUSHA AJALI

Rais Mstaafu wa Awamu ya Pili, Ali Hassan Mwinyi, akisikiliza maelezo kutoka kwa Inspekta Ibrahim Samwix, wakati alipotembelea mabanda mbalimbali kwenye Tamasha la Usalama Barabarani lililofanyika Uwanja wa Uhuru, jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Naibu Waziri Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mwenyekiti wa Baraza la Taifa la Usalama Barabarani, Mhandisi Hamad Masauni.Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi
Rais Mstaafu wa Awamu ya Pili, Ali Hassan Mwinyi (aliyevaa suti), akisikiliza maelezo jinsi uvunjaji wa sheria za usalama barabarani unavyoweza kusababisha ajali, wakati alipotembelea banda la Maaskari wa usalama barabarani, kwenye Tamasha la Usalama Barabarani lililofanyika jana Uwanja wa Uhuru, jijini Dar es Salaam.
Naibu Waziri Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mwenyekiti wa Baraza la Taifa la Usalama Barabarani, Mhandisi Hamad Masauni (kushoto), akimkabidhi tuzo Mgeni Rasmi, Rais Mstaafu wa Awamu ya Pili, Ali Hassan Mwinyi, wakati wa Tamasha la Usalama Barabarani lililofanyika jana Uwanja wa Uhuru, jijini Dar es Salaam.
Kamishna wa Operesheni na Mafunzo wa Jeshi la Polisi, Nsato Marijani (kushoto), akipokea zawadi kutoka kwa Naibu Waziri Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mwenyekiti wa Baraza la Taifa la Usalama Barabarani, Mhandisi Hamad Masauni kwa niaba ya Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, IGP Simon Sirro kwa kutambua mchango wake katika suala nzima la Usalama Barabarani wakati wa Tamasha la Usalama Barabarani lililofanyika jana, Uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam.Kulia ni Rais Mstaafu wa Awamu ya Pili, Ali Hassan Mwinyi.
Balozi wa Usalama Barabarani, Samira Abuu (katikati), akiwa katika picha ya pamoja na Mgeni Rasmi, Rais Mstaafu wa Awamu ya Pili, Ali Hassan Mwinyi na Naibu Waziri Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi,Mwenyekiti wa Baraza la Taifa la Usalama Barabarani,Mhandisi Hamad Masauni, baada ya kupokea cheti cha kutambua mchango wake katika masuala ya Usalama Barabarani wakati wa Tamasha la Usalama Barabarani lililofanyika jana, Uwanja wa Uhuru, jijini Dar es Salaam.
Mgeni Rasmi,Rais Mstaafu wa Awamu ya Pili, Ali Hassan Mwinyi, akizungumza wakati wa Tamasha la Usalama Barabarani ambapo aliwaasa watumiaji wa vyombo vya moto kufuata sheria za usalama barabarani ili kuepuka ajali zinazosababisha ulemavu na vifo.Tamasha hilo limefanyika jana, Uwanja wa Uhuru, jijini Dar es Salaam. 

IMEANDALIWA NA KITENGO CHA MAWASILIANO SERIKALINI-WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI.

No comments: