Advertisements

Friday, September 1, 2017

MSAADA WA HARAKA UNAHITAJIKA BADO KIDOGO TUTAFIKIA LENGO

Ndugu zetu Watanzania tunasikitika kuwafahamisha kuwa ndugu yetu na kaka yetu Meya Mlima (pichani juu)anashikiliwa na ICE (Immigration) tokea mwisho mwa wiki iliyopita huko New Hampshire.

Mpaka muda huu marafiki na wanafamilia ya Meya wanafuatilia kesi yake ili kujua jinsi gani tunaweza kumsaidia pamoja na kujua gharama za mwanasheria pia kujua mchakato mzima wa kesi itakavyosikilizwa.

Kamati inapenda kuwafahamisha marafiki, ndugu, na jamaa wa Meya kuwa kutahitajika msaada wa Pesa ili ndugu yetu aweze kutoka na kuendelea kuwalea vijana wake na kushiriki nasi katika gurudumu la maisha ya huku ughaibuni.

Kwa sasa Familia na kamati wako katika mchakano wa kupata mwanasheria mwenye uzoefu katika maswala ya uhamiaji (immigration) . Kamati na Familia itaendelea kuwafahamisha kila hatua itakayo piga katika kumsaidia ndugu yetu Meya Mlima

Kwa ushauri na maelezo zaidi wasiliana na wafuatao:

Babie Mgaza 2022005031
Raju Tambwe 4433177440
Jasmine Rubama 4103719966
Mganga Muhombolage 2023740988
Iddi sandaly 3016135165
Kessy Metro tires 2024135933
Jabir Jongo 2406040574

UNAWEZA KUTOA MSAADA WAKO HAPA TAFADHALI FAMILIA NA KAMATI INATANGULIZA SHUKURANI

KWA KUCHANGIA BOFYA HAPA

SHUKURANI KUTOKA KWA MAMA MZAZI WA MAYOR

7 comments:

Anicetus said...

Safari ya kuja huku ugagibuni ni ndefu na ina faida and madahara yake. Mtu huwezi kujua utapata ajali gani au bahati ya maisha mazuri. Huyu ndugu yetu hakupanga kupata matatitizo, bali binadanu ndivyo tulivo. Kwenye safafri hii, mnoja wetu akianguka ni lazima wote tumuinue.

Anonymous said...

Wana UGAIBUNI wote shikamaneni sana kwa umoja kama Watanzania na Wazalendo ili Ndg Mlima atoke. Msiangalie dini , utaifa na kabila.

Tumaini Geofrey Temu said...

Mayor Mtu wa watu hawezi achwa mwenyewe kamwe

Anonymous said...

Anashikiliwa kwa kisa gani haswa???maana maelezo yapo nusu nusu

Anonymous said...

Watu wote wana diaspora, Mungu awabariki sana nyote kwa kushikamana ktk kila jambo. Mliopo Mehco, USA na Canada mmetupatia somo kubwa sana kwa sisi wengine tuliopo Ulaya, Australia na Africa. Mea ni mtu wa watu tunaamini atatoka na siku moja atapata haki zake zote za kuishi huko bila bughdha.

Unknown said...

Maelezo yaliyotolewa katika tangazo hili yanajitosheleza na yanatosha. Tufanyeni kila linalowezekana tumkwamue kijana wetu. Meya ni mtu wa watu hasa.

Anonymous said...

Mpaka leo hii almost a month tangu tangazo la kwanza litoke bado mchakato wa kutafuta lawyer unaendelea? Are we really serious?