Advertisements

Tuesday, March 20, 2018

MAKAMU WA RAIS SAMIA SULUHU KUWAKILISHWA NA DKT. MWIGULU NCHEMBA KATIKA TAMASHA LA PASAKA 2018 KANDA YA ZIWA

Mkurugenzi wa Msama Promotions, Alex Msama akitoa ufafanuzi juu ya ujio wa mgeni rsmi ambaye ni Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano Mhe. Samia Suluhu ambaye atawakilishwa na  Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Dkt. Mwigulu Nchemba. Pembani ni Mtatibu wa Tamasha hilo, Jimmy Charles (kushoto).

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu anatarajia kuwa mgeni rasmi katika Tamasha la Pasaka 2018 linalotarajiwa kufanyika Kanda ya Ziwa ambapo Aprili 1 itakuwa Uwanja wa CCM-Kirumba na Aprili 2, 2018 ni Simiyu.
Mkurugenzi wa Msama Promotions, Alex Msama ameyasema hayo leo wakati akiongea na wanahabari jijini Dar es Salaam kuwa wamejiandaa vya kutosha na Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu atawakilishwa na Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Dkt. Mwigulu Nchemba.
"Sisi tumejiandaa vya kutosha Tamasha la Kutosha Mwaka huu ni moto hakuna haja ya kukosa kuhudhuria, waimbaji wamejiandaa vya kutosha kila na upande wa usalama umekamilika vizuri," anasema Msama.
Waandishi wa habari wakifuatilia mkutano huo.

No comments: