Advertisements

Monday, July 23, 2018

BINTI WA MIAKA 15 AFUNGWA KWA KUTOA MIMBA ALIYOBAKWA NA KAKA’KE

Related image
BINTI wa miaka 15 nchini Indonesia amefungwa miezi sita kwa kutoa mimba aliyoipata baada ya kubakwa mara nane na kaka yake.

Kwa mujibu wa gazeti la Hindustan Times, hukumu hiyo ilifikiwa katika kesi ya siri katika mahakama ya Wilaya ya Muara Bulian kwenye kisiwa cha Sumatra, kwani sheria za Indonesia zinapiga marufuku utoaji mimba, isipokuwa tu kwa mwanamke ambaye maisha yake yako hatarini.

Kwa msichana huyo, ilibidi aitoe mimba hiyo kabla ya kufikia miezi sita.

Mama wa binti huyo aliyemsaidia kuitoa naye anakabiliwa na mashitaka kwa kushiriki tukio hilo.-GPL

No comments: