Advertisements

Wednesday, January 9, 2019

*DAR ES SALAAM TUNASEMA HAACHWI MTU*.



RC MAKONDA AWAHAKISHIA WANAFUNZI 31,092 SAWA NA 47% YA WATOTO 64,861 WALIOFAULU KATIKA MKOA WA DAR ES SALAAM KUENDELEA NA MASOMO YAO*.
Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam *Mhe. Paul Makonda* amewahakikishia *wanafunzi 31,092* sawa na *47%* ya watoto *64,861* ambao walifaulu katika mkoa huo kuendelea na masomo yao ya *kidato cha kwanza* kwakuwa serikali imeanza *ujenzi na ukarabati* wa vyumba vya *madarasa 622* ili kuhakikisha *hakuna mwanafunzi atakaeachwa* kwa kigezo cha *uhaba wa madarasa.*
*RC Makonda* amesema *ongezeko la wanafunzi na ufaulu* ni matokeo ya mafanikio ya *Rais Dkt. Magufuli* kutenga fedha zaidi ya *bilioni 29* kwaajili ya *elimu Bure* ambapo kati ya hizo *Bilioni 17.46* zinaenda kwenye *elimu ya sekondari* na tayari *Serikali imejipanga* na kuhakikisha kuwa tangu *January 07 shule zote 147 za sekondari zimefunguliwa* hivyo *kila mzazi ahakikishe anamuandikisha mtoto* ili kuendelea na kidato cha Kwanza.

Aidha *RC Makonda* amesema katika matokeo ya mtihani wa *Darasa la Saba* mkoa huo umekuwa *kinara* kwa kufaulisha *wanafunzi 64,861* sawa na *92%* ambapo kati ya hao Wanafunzi *31,092* walikosa *vyumba vya madarasa* jambo lililoilazimu serikali kupambana kuhakikisha *kila aliefaulu anaendelea na masomo.*

Hata hivyo *RC Makonda* amesema lengo la *ujenzi wa madarasa* hayo ni kuhakikisha kila mwanafunzi anatumia *fursa ya Elimu Bure* iliyotolewa na *Rais Dkt. John Magufuli* ya kuhakikisha *Mtoto wa maskini anasoma* ili kujikwamua *kiuchumi* na mwisho wa siku Taifa liwe na *wataalamu wa kutosha.*

Pamoja na hayo *RC Makonda* amewaonya wanafunzi *watakaokwepa kusoma* watakamatwa na kuchukuliwa *hatua kali za kisheria*.

*DAR ES SALAAM TUNASEMA HAACHWI MTU*.




No comments: