Advertisements

Monday, March 25, 2019

SPIKA NDUGAI AGAWA VITABU SHULE ZA SEKONDARI WILAYANI KONGWA

Spika wa Bunge na Mbunge wa Kongwa, Job Ndugai akiwaonyesha moja ya vitabu alivyowapatia wanafunzi wa Shule ya  Sekondari Banyi Banyi wakati wa ziara ya kikazi jimboni kwake na kuwagawia vitabu na jezi tukio lililofanyika  tarehe 24 Machi, 2019 Wilayani Kongwa Mkoani Dodoma.
Wanafunzi wa Shule ya Sekondari Banyi Banyi wakimsikiliza Spika wa Bunge na Mbunge wa Kongwa, Job Ndugai (hayupo kwenye picha) alipoitembelea Shule hiyo katika ziara yake ya kutembelea Shule mbali mbali zilizopo Wilayani Kongwa na kugawa vitabu, jezi, mipira, Komputa na Printa kwa wanafunzi wa shule hizo tukio lililofanyika tarehe 24 Machi, 2019 Wilayani Kongwa Mkoani Dodoma.
Spika wa Bunge na Mbunge wa Kongwa, Job Ndugai akisaini kitabu cha wageni wakati alipotembelea Shule ya Sekondari Banyi Banyi wakati wa ziara ya kikazi Jimboni kwake tarehe 24 Machi, 2019 Wilayani Kongwa Mkoani Dodoma.
Spika wa Bunge na Mbunge wa Kongwa, Job Ndugai akiwauliza maswali wanafunzi wa kidato cha pili na cha nne wa Shule ya Sekondari Songambele Kilimani wakati wa ziara yake ya kikazi jimboni kwake na kuwagawia vitabu tukio lililofanyika tarehe 24 Machi, 2019 Wilayani Kongwa Mkoani Dodoma.
Spika wa Bunge na Mbunge wa Kongwa, Job Ndugai (kushoto) akimkabidhi mpira Mwalimu Mkuu wa Shule ya Sekondari Ndelibo, Ndg. Christina Uhengo wakati wa ziara yake ya kikazi jimboni kwake na kuwagawia vitabu na jezi tukio lililofanyika tarehe 24 Machi, 2019 Wilayani Kongwa Mkoani Dodoma.
Spika wa Bunge na Mbunge wa Kongwa, Job Ndugai akimkabidhi printa Mwalimu Mkuu wa Shule ya Sekondari Ibwaga wakati wa ziara ya kikazi jimboni kwake na kuwagawia vitabu na jezi tukio lililofanyika tarehe 24 Machi, 2019 Wilayani Kongwa Mkoani Dodoma.
Spika wa Bunge na Mbunge wa Kongwa, Job Ndugai akizungumza na wanafunzi wa Shule ya Sekondari Hogoro wakati wa ziara ya kikazi jimboni kwake na kugawa vitabu, jezi na mipira tukio lililofanyika tarehe 24 Machi, 2019 Wilayani Kongwa Mkoani Dodoma.
Spika wa Bunge na Mbunge wa Kongwa, Job Ndugai (alieshika Kofia) katika picha ya pamoja na walimu na wanafunzi wa kidato cha II Shule ya  Sekondari Hogoro wakati wa ziara ya kikazi jimboni kwake na kugawa vitabu na jezi tukio lililofanyika tarehe 24 Machi, 2019 Wilayani Kongwa Mkoani Dodoma.
(PICHA NA OFISI YA BUNGE)

No comments: