Monday, October 12, 2020

MAADHIMISHO YA SIKU YA CHAKULA DUNIANI YAINGIA SIKU YA TATU MKOANI NJOMBE

Kaimu Mkurugenzi Idara ya Usalama wa Chakula Dkt.Honest Kessy akitazama chupa ya dawa ya kuhifadhi mahindi iliyotengenezwa na kamapuni ya Mtewele General Traders Njombe wakati wa maadhimisho ya siku ya Chakula Duniani kitaifa mkoani Njombe leo.Kulia ni Afisa Masoko Benedicto Mgaya wa Mtewele Traders.
Kaimu Mkurugenzi Usalama wa Chakula toka Wizara ya Kilimo Dkt.Honest Kessy (aliyevaa miwani) akipata maelezo ya bidhaa za wajasiliamali wa wilaya ya Makete zilizoongezwa thamani wakati alipomwakilisha Katibu Mkuu Wizara ya Kilimo kutembelea mabanda ya maonesho ya siku ya chakula .Katikati ni Afisa Kilimo toka Halmashauri ya Wilaya ya Makete Amon Mhagama akitoa maelezo kwa mgeni rasmi .
Kaimu Mkurugenzi Mkuu Idara ya Usalama wa Chakula Wizara ya Kilimo Dkt.Honest Kessy (aliyeva kofia kulia) akitazama teknolojia ya kumwagilia mazao kwa njia ya asili kutumia kisima iliyotengenezwa na kikundi cha Uvinjo Njombe.Kushoto ni Meneja Mradi wa Uvinjo Dauson Msumange leo ikiwa ni siku ya tatu ya maadhimisho ya Siku ya Chakula kitaifa mkoani Njombe.
Meneja wa Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF) Mkoa wa Njombe Mrisho Mwisimba ( kulia) akikabidhi zawadi ya nyaraka za huduma zitolewazo na shirika hilo kwa wakulima kwa mwakilishi wa Katibu Mkuu Wizara ya Kilimo ambaye pia ni Kaimu Mkurugenzi Idara ya Usalama wa Chakula Dkt.Honest Kessy (kushoto) alipotembelea banda hilo leo ikiwa ni siku ya Tatu ya maonesho ya Siku ya Chakula Duniani kitaifa mkoani Njombe.
Kaimu Mkurugenzi Idara ya Usalama wa Chakula ambaye pia ni mwakilishi wa Katibu Mkuu Wizara ya Kilimo Dkt.Honest Kessy (kushoto) akipokelewa na wajumbe wa kamati ya mandalizi ya siku ya Chakula Duniani Kitaifa inayofanyik Njombe leo alipowasili uwanja wa maonesho kwa kazi ya kukagua mabanda na kuongea na wakulima

(Picha na Wizara ya Kilimo)

Maonesho ya Siku ya Chakula Duniani Kitaifa mkoani Njombe yamefikia siku ya tatu mkoani Njombe ambapo mapema leo ilikuwa zamu ya Katibu Mkuu Wizara ya Kilimo Bw. Gerald Kusaya kutembelea mabanda ya maonesho na kuzungumza na wakulima na wajasiliamali waliopo.

Hata hivyo Katibu Mkuu amewakilishwa na Kaimu Mkurugenzi Idara ya Usalama wa Chakula Dkt.Honest Kessy ambaye amewapongeza wakulima,wafugaji na wajasiliamali kwa kujitokeza kwa wingi kushiriki kwenye maonesho ya mwaka huu.
” Wizara ya Kilimo inawapongeza wakulima ,wafugaji na wajasiliamali nchini kwa kazi kubwa mnayofanya ya kuhakikisha nchi inakuwa na uhakika wa chakula muda wote hali inayofanya uchumi wetu ukue” alisema Dkt.Kessy

Siku ya Chakula Duniani ilifunguliwa tarehe 10 Octoba na itafikia kilele tarehe 16 Octoba ikiongozwa na kauli mbiu isemayo ” Kesho Njema Itajengwa na Lishe Bora Endelevu”

No comments:

Post a Comment

bila kutumia lugha ya matusi na kumharibia mtu siku
yake