Advertisements

Wednesday, September 22, 2021

WAKUU WA TAASISI SEKTA YA UCHUKUZI WASAINI MKATABA WA UTENDAJI KAZI

Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi (Sekta ya Uchukuzi), Bw. Gabriel Migire, akizungumza na Menejimenti ya Wizara na Wakuu wa Taasisi wakati wa halfa ya kusaini mikataba ya utendaji kazi kati ya Wizara na Taasisi 14 zilizopo chini ya Sekta hiyo, jijini Dodoma.
Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Sera na Mipango kutoka Sekta ya Uchukuzi, Bi. Naima Mrisho, akitoa taarifa kwa Menejimenti na Wakuu wa Taasisi 14 zilizo chini ya Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi (Sekta ya Uchukuzi), katika kikao kazi cha utiaji saini wa utendaji kazi, jijini Dodoma.
Afisa Usafirishaji Mkuu Sekta ya Uchukuzi, Bw. Alphonce Mwingira, akitoa maoni katika kikao kazi cha Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi (Sekta ya Uchukuzi), kilichowakutansha Menejimenti na Wakuu wa Taasisi 14 wa Sekta hiyo, jijini Dodoma.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi (Sekta ya Uchukuzi), Bw. Gabriel Migire, akisaini mkataba wa utendaji kazi na Wakuu wa Taasisi 14 zilizo chini ya Sekta hiyo katika ofisi za Wizara Mtumba, jijini Dodoma.

PICHA NA WUU

No comments: