Advertisements

Monday, November 22, 2021

Ole Gunner Afukuzwa Manchester United

HATIMAYE Klabu ya Manchester United imefikia makubaliano ya kuachana na kocha wake Ole Gunner Solskjaer, hatua hiyo inafuatia matokeo mabaya mfululizo ikiwemo kipigo cha 4-1 kutoka kwa Watford Jumamosi ya Novemba 20.

Baada ya saa 5 za mazungumzo hatimaye pande zote zimekubaliana kuvunja mkataba huo, timu kwa sasa itakuwa chini ya viungo wa zamani wa klabu hiyo Michael Carrick na Fletcher.

Mpaka sasa Zinedine Zidane ndiye chaguo namba moja kuwa mbadala wa Ole Gunnar Solskjaer.

No comments: