Advertisements

Saturday, May 4, 2024

MAADHIMISHO YA SIKU YA UHURU WA VYOMBO VYA HABARI YAFANYIKA ZANZIBAR.


Mkurugenzi Idara ya Utalii Dkt,Abdalla Mohamed Juma akitoa mada ya Historia ya vyombo vya Habari Zanzibar katika hafla ya Kongamano la Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari lililofanyika katika ukumbi wa Sanaa Rahaleo Zanzibar.
Afisa Sheria Tume ya Utangazaji Zanzibar Khadija Mabrouk Hassan akitoa mada ya Mabadiliko ya Sera Sheria na Kanuni za Habari Zanzibar katika hafla ya Kongamano la Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari lililofanyika katika ukumbi wa Sanaa Rahaleo Zanzibar.
Katibu Mkuu wizara ya Habari Vijana Utamaduni na Michezo Fatma Hamadi Rajab akitoa hotuba katika hafla ya Kongamano la Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari lililofanyika katika ukumbi wa Sanaa Rahaleo Zanzibar.
Afisa Mwandamizi Baraza la Habari Tanzania Ofisi ya Zanzibar Shifaa Said Hassan akichangia mada katika hafla ya Kongamano la Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari lililofanyika katika ukumbi wa Sanaa Rahaleo Zanzibar.
Prof,Jennifer Thomas kutoka Howard University Washington akizungumza katika hafla ya Kongamano la Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari lililofanyika katika ukumbi wa Sanaa Rahaleo Zanzibar.
Mkurugenzi Mstaafu Idara ya Habari Maelezo Yussuf Omar Chunda akitoa neno la Shukurani katika hafla ya Kongamano la Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari lililofanyika katika ukumbi wa Sanaa Rahaleo Zanzibar.
Msemaji wa Ubalozi wa Marekani Dar es salaam Kalisha Holmes akizungumza katika hafla ya Kongamano la Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari lililofanyika katika ukumbi wa Sanaa Rahaleo Zanzibar.



Na Khadija Khamis – Maelezo .04/05/2024.

Serikali ya Mapinduzi Zanzibar imesema inaendelea kuweka mazingira mazuri kwa waandishi wa habari kwa kuzingatia sheria na sera na kanuni zilizopo ili kuwawezesha kufanya kazi zao kwa ufanisi.

Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Fatma Hamad Rajab alisema hayo kwa niaba ya Waziri wa Wizara hiyo wakati wa maadhimisho ya Uhuru wa Vyombo vya Habari katika ukumbi wa Sanaa Rahaleo.

Alisema hatua hiyo inakuja kwa kufuata sera na kanuni za habari kwa kuweka mazingira bora kwa waandishi ili kutekeleza vyema kazi zao.

Alifahamisha kuwa vyombo vya habari vinamchango mkubwa wa kuchochea maendeleo ya nchi hivyo ni vyema kutumia maadili na uweledi katika utekelezaji wa kazi zao.

Alisema mwaka 1993 Baraza kuu la Umoja wa Mataifa ilianzisha siku ya uhuru wa vyombo vya habari ili kukuza na kuendeleza haki na uhuru wa habari kwasababu dunia ikizingatia nyenzo muhimu ya maendeleo kupitia Nyanja mbalimbali.

Sambamba na hayo alisema tume ya utangazaji inajukumu la kutoa leseni kwa wawekezaji wenye uwezo wa kuanzisha vyombo vya habari kwa kuzingatia sera na sheria za vyombo vya habari.

Akiwasilisha mada ya Historia ya vyombo vya habari Mkurugenzi wa Idara ya Utalii na Mambo ya Kale, Dkt. Abdalla Mohammed Juma alisema Zanzibar inahistori refu kwa masuala ya mawasiliano kuliko nchi nyengine duniani.

Alisema Zanzibar ni nchi ya mwanzo kusini mwa jangwa la sahara kuwa na simu inayotumia wayalesi, kiwanda cha uchapishaji na Televisheni ya rangi, sinema na makapuni na vyombo vya habari lakini bado kwa sasa kuna changamoto kwa baadhi ya waandishi kutekeleza majukumu yao ipasavyo.

Nae Ofisa Sheria wa Tume ya Utangazaji Zanzibar Khadija Mabrouk Hassan alipokuwa akiwasilisha mada ya mabadiliko ya sera, sheria na kanuni za habari Zanzibar alisema sekta ya habari ni muhimili mkuu katika kuchochea maendeleo ya nchi kutokana na kutoa haki ya msingi ya kikatiba.

Alisema sekta ya habari hapa nchini inasimamiwa na sheria ili kuwawezesha waandishi kutekeleza majukumu yao kwa uweledi.

Kaulimbiu ya Maadhimisho ya uhuru wa vyombo vya habari ni ‘Uwandishi wa Habari na Changamoto ya Mabadiliko ya Tabia Nchi’.



No comments: