ANGALIA LIVE NEWS

Wednesday, March 31, 2010

Afisa ubalozi, mgeni rasmi Simba na Yanga,Dc


                      Simba (Lunyasi)


Afisa ubalozi amekubali mualiko kuwa mgeni rasmi kwenye kindumbwe dumbwe cha Simba na Yanga,mechi inayozungumziwa mjini Washinngton na vitongoji vyake,
                                           Yanga Imara



Mpambano huo wa kukata na shoka utachezwa jumapili April 4 kwenye wanja jipya la 1417 Kalmia St,Nw,Washington Dc,kambi zote zipo shwari na zinaendelea vizuri na mazoezi.Simba inaonekana imejiimarisha zaidi baada ya wachezaji wengi wa mikoani akiwemo Francis Makalaa aliyewahi kuichezea Simba miaka ya Nyuma kuthibitisha kuwepo kwenye mpambano huo,Kuhusu Nteze John bado viongozi wa Simba wanaendelea kumtafuta kwa udi na uvumba,Nteze anaishi Washington State alisahawahi  kua mchezaji wa kutumainiwa Simba na Timu ya Taifa.kabla hajajiunga na Simba,alikua mchezaji wa Pamba ya Mwanza.

                             Stars United

Kambi ya Yanga imekua kimya Kocha Yasini Randi amesema Simba wacha waongee,msema ukweli dakika 90,sisi bwana tupo tunaendelea vizuri na kambi yetu,sisi tunaingia uwanjani kama YANGA IMARA KUFUNGWA DAIMA MWIKO

Jumamosi April 3 kutakua na mechi nyingine ya Stars na Maryland untd,itakayochezewa 

18031 central park circle,
 Boyds,Md,20841,uwanja # 20

mechi hii ni moja ya mechi za kujinoa ya Stars kwa safari ya kuelekea Sweden july mwaka huu,mechi nyingine ya Stars ni April 24 mjini Boston itapambana na Zambia
                    Maryland United

No comments: