ANGALIA LIVE NEWS

Tuesday, May 17, 2011

Strauss-Kahn akana mashtaka

Mkuu wa IMF Dominique strauss-Kahn (katikati) akitolewa katika kituo cha polisi mjini New York juzi
NEW YORK, Marekani 
MKUU wa Shirika la Fedha Ulimwenguni (IMF), Dominique  Strauss Kahn  amefikishwa mahakamani  mjini  New York kwa madai ya matumizi ya nguvu kushinikiza kitendo kumwingilia kimwili mhudumu wa chumba katika hoteli moja  ya kifahari. 

Kahn amefikishwa mahakamani ambapo amekana mashtaka yote dhidi yake na kwa mujibu wa wakili wake, mteja wake alikabidhi nguo zake kwa ajili ya  uchunguzi wa DNA. 

Wakili huyo, William Taylor alisema mkuu huyo wa shirika la IMF alikanusha madai hayo ya kumshambulia mwanamke huyo kwa nia ya kufanya nae mapenzi pamoja na jaribio la kumbaka. 

Polisi mjini New York ilisema kuwa Kahn hana haki ya kidiplomasia kumzuia  asishtakiwe na kwamba iwapo atathibitishwa kuwa na hati, anaweza kufungwa  miaka 15 hadi 20 jela. 

IMF imemtaja John Lipsky kuwa kaimu mkurugenzi mkuu na kusema kuwa Nemat  Shafik, naibu mkurugenzi mkuu ambaye anahusika na usimamizi wa kazi za IMF  katika mataifa kadhaa ya Ulaya, atahudhuria mkutano wa jana Jumatatu mjini  Brussels badala ya Strauss-Kahn.

AFP

No comments: