ANGALIA LIVE NEWS

Thursday, April 12, 2012

TANGAZO MAALUMU LA MKUTANO WA JUMUIYA YA WATANZANIA DMV TAREHE APRIL/15/2012

Ndugu Wanajumuiya,
Kama tulivyowafahamisha hapo awali kuwa kazi mliyotutuma imekamilishwa. Tuna washukuruni wote mlioleta na kutuma mapendekezo yenu kutokea mwanzo mpaka mwisho wa ukamilishaji wa Katiba mpya. Maoni yenu yote yalipokelewa na kufanyiwa kazi ndani ya Katiba, tunashukuru sana kwa mchango na muda wenu mliojitolea kwa nia ya kujenga Jumuiya yetu ya Watanzania DMV.
Hivyo basi, imetufikisha katika hatua kubwa naya mwisho ya kuindeleza mbele Jumuiya yetu. Na kama tunavyojua kuwa kwa sasa hivi hatuna Jumuiya na kamati iliyofanyia marekebisho katiba haina Fedha, Kutokana na hali hiyo, Wanakamati tumependekeza  kama ifuatavyo
-          Tutakuwa na Mkutano mkuu mmoja ambao utashughulikia maswala makuu mawili:

1.      Shughuli ya kwanza itakuwa ya kupitia na kupitisha Katiba.

2.      Shughuli ya pili itakuwa ya uchaguzi mkuu, tutachagua viongozi wa Jumuiya.

Mkutano Mkuu utafanyika tarehe  04/15/2012  saa 8 mchana ( 2:00pm).  Katika
Ukumbi wa  
MIRAGE HALL
1401 UNIVERSITY BLVD
HYATTSVILLE, MD 20783

1 comment:

Daudi said...

DJ...siku hiyo tutahitaji kuchagua kamati ya uchaguzi...kamati iliyopo sasa ilipewa jukumu la kusimamia katiba na sio uchaguzi. Hatuna imani nayo kwani kiongozi wake tayari amemuindozi mmoja wa wagombea. Ongeza hili kama moja ya ajenda ya jumapili.

Mdau DMV