Kamanda wa Kikosi cha Kupambana na Kudhibiti Madawa ya Kulevya
nchini, Godfrey Nzowa akionyesha madawa yaliyokamatwa na kumuhusisha
Abdullalatif Fundikira.
Kamanda Nzowa alisema kuwa jeshi lake limelazimika kumkamata Fundikira
baada ya kuwa katika orodha ya watu waliotajwa kujihusisha na biashara
haramu ya madawa ya kulevya.
Aliongeza kuwa mtuhumiwa huyo alidakwa nyumbani kwake, Mbezi Beach, Kinondoni Jijini Dar es Salaam saa 12.00 asubuhi.
“Fundikira tulimkamata nyumbani kwake, ilikuwa saa kumi na mbili asubuhi. Kwa sasa tunamshikilia na upelelezi unaendelea, utakapokamilika atafikishwa mahakamani kujibu tuhuma zinazomkabili,” alisema Kamanda Nzowa.
Akaongeza: “Fundikira alikuwa akitafutwa na jeshi tangu Mei 16 mwaka huu baada ya kutajwa na mwanamke mmoja anayejulikana kwa jina la Mariam Mohamed Said, 29, kuwa ni miongoni mwa wauza madawa ya kulevya.
“Huyu mwanamke alinaswa katika Uwanja wa Ndege wa Mwalimu Julius Nyerere katika operesheni ya polisi ya ‘kufagia’ mtandao wa madawa ya kulevya.”
“Fundikira tulimkamata nyumbani kwake, ilikuwa saa kumi na mbili asubuhi. Kwa sasa tunamshikilia na upelelezi unaendelea, utakapokamilika atafikishwa mahakamani kujibu tuhuma zinazomkabili,” alisema Kamanda Nzowa.
Akaongeza: “Fundikira alikuwa akitafutwa na jeshi tangu Mei 16 mwaka huu baada ya kutajwa na mwanamke mmoja anayejulikana kwa jina la Mariam Mohamed Said, 29, kuwa ni miongoni mwa wauza madawa ya kulevya.
“Huyu mwanamke alinaswa katika Uwanja wa Ndege wa Mwalimu Julius Nyerere katika operesheni ya polisi ya ‘kufagia’ mtandao wa madawa ya kulevya.”

No comments:
Post a Comment