![]() |
| Mkurugenzi wa Misitu na Nyuki Dk. Felician Kilahama |
Watumishi wawili wa Idara ya Misitu waliokuwa doria katika msitu wa asili wa Shengena ulioko wilayani Same mkoani Kilimanjaro, wamenusurika kuuawa baada ya kuzingirwa na kundi la watu wanachiimba madini katika msitu huo.
Kaimu Mkuu wa hifadhi ya msitu huo, Halifayo Ngoma, amesema watumishi hao walikumbwa na mkasa huo mwanzoni mwa wiki hii baada yakukutana na kundi la watu zaidi ya 50 na kuwazingira.
Ngoma alifafanua kuwa watumishi hao walifanikiwa kutoroka na kujiokoa na janga hilo.
Aidha, Ngoma pamoja na kuiomba kuiomba serikali kusaidia kupunguza changamoto zinazowakabili kwa kuongeza watumishi na vitendea kazi, alisema hili ni tukio la pili la kushambuliwa na majangili hao ambao wamefanya uharibifu mkubwa katika vyanzo vya maji ambavyo asilimia kubwa vimeharibiwa na kemikali zinazotumika kutafuta madini hayo.
Alisema kuwa mara ya kwanza majangili hao walishawashambulia kwa kuwarushia mishale na wamesisitiza umuhimu wa serikali kuchukua tahadhari kabla ya hatari kwani hali ni mbaya.
Akizungumza baada ya kutembelea na kujionea uharibifu mkubwa wa mazingira, Mkurugenzi wa Misitu na Nyuki Dk. Felician Kilahama, pamoja na kuitaka kamati ya ulinzi na usalama ya Wilaya ya Hai kuwatafuta wote wanaotishia maisha ya watumishi hao, amekiri kuwa hali katika msitu huo ni mbaya na kwamba sasa watalazimika kuchukua maamuzi magumu.
“Hatuwezi kuendelea kuangalia mambo haya yanatokea, ni lazima hatua zichukuliwe na ikibidi hata maamuzi magumu kwani vitendo hivi sasa havivumiliki,” alisema Kilahama.
Mkuu wa Wilaya ya Same, Hermani Kapufi, na Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Same, Christopher Irira pamoja na kutoa mapendekezo mbalimbali yanayolenga kudhibiti vitendohivyo, wamesema wameshaanza kuwatafuta.
Kaimu Mkuu wa hifadhi ya msitu huo, Halifayo Ngoma, amesema watumishi hao walikumbwa na mkasa huo mwanzoni mwa wiki hii baada yakukutana na kundi la watu zaidi ya 50 na kuwazingira.
Ngoma alifafanua kuwa watumishi hao walifanikiwa kutoroka na kujiokoa na janga hilo.
Aidha, Ngoma pamoja na kuiomba kuiomba serikali kusaidia kupunguza changamoto zinazowakabili kwa kuongeza watumishi na vitendea kazi, alisema hili ni tukio la pili la kushambuliwa na majangili hao ambao wamefanya uharibifu mkubwa katika vyanzo vya maji ambavyo asilimia kubwa vimeharibiwa na kemikali zinazotumika kutafuta madini hayo.
Alisema kuwa mara ya kwanza majangili hao walishawashambulia kwa kuwarushia mishale na wamesisitiza umuhimu wa serikali kuchukua tahadhari kabla ya hatari kwani hali ni mbaya.
Akizungumza baada ya kutembelea na kujionea uharibifu mkubwa wa mazingira, Mkurugenzi wa Misitu na Nyuki Dk. Felician Kilahama, pamoja na kuitaka kamati ya ulinzi na usalama ya Wilaya ya Hai kuwatafuta wote wanaotishia maisha ya watumishi hao, amekiri kuwa hali katika msitu huo ni mbaya na kwamba sasa watalazimika kuchukua maamuzi magumu.
“Hatuwezi kuendelea kuangalia mambo haya yanatokea, ni lazima hatua zichukuliwe na ikibidi hata maamuzi magumu kwani vitendo hivi sasa havivumiliki,” alisema Kilahama.
Mkuu wa Wilaya ya Same, Hermani Kapufi, na Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Same, Christopher Irira pamoja na kutoa mapendekezo mbalimbali yanayolenga kudhibiti vitendohivyo, wamesema wameshaanza kuwatafuta.
CHANZO: NIPASHE

No comments:
Post a Comment