ANGALIA LIVE NEWS

Friday, August 3, 2012

NGASSA AANZA MAZOEZI SIMBA



siku mbili baada ya  kuzusha taflani kufuatia sakata la uhamisho kutoka timu yake ya zamani ya Azm Fc, nyota wa klabu ya Simba Mrisho ngasa ameanza mazoezi rasmi asubihi ya leo mara baada ya kukamilika kwa taratibu za usajili wake   mapema  jana.

Akizungumza na teentz.com muda mfupi baada ya kumaliza  mazoezi hayo Ngasa amedokeza kuwa  anataka kufanya mambo makubwa akiwa na timu yake hiyo mpya na amewaomba mashabiki wa Simba  kumuamini na kumpa ushirikianao.

"sina kingine, nataka kufanya makubwa nikiwa na timu yangu mpya naomba mashabiki waniamini na kunipa ushirikiano" alisema

Ngassa  amejiunga na Simba  na  kukabiziwa  jezi namaba 16 sambamba na ndinga ya kisasa aina ya Verossa huku akilamba shavu la kuvuta mshahara wa shilingi za kibongo Milioni 2 kwa Mwezi
STORI NA  DISMAS TEN 0718489260.

No comments: