Advertisements

Friday, August 10, 2012

NI MAJONZI: MAMIA WAJITOKEZA KUAGA MWILI WA ASKARI ALIYEJINYONGA MORO



 Mtoto Consolatha Donald (7) akiaga mwili wa marehemu baba yake huku akiwa mikononi mwa mama yake mzazi Diana.

Mjane Diana akiangua kilio baada ya kutoa heshima za mwisho mbele ya mwili wa aliyekuwa mume wake Afande Donald Mathew

Mchungaji akiongoza ibada ya mazishi
 
Mwandishi wa Gazeti la Mwananchi Hamida Shariff akimpa pole mke wa marehemu Diana 

Danstan Shekidele, Morogoro yetu

Mamia wajitokeza jioni hii kuaga mwili wa askari Donald Mathew Dunga aliyefariki baada ya kujinyonga juzi kwenye daraja la shani mjini Morogoro.

Mwili wa askari huyo umeagwa jioni hii katika jioni hii kwenye chumba cha kuhifadhia maiti cha hospital ya Mkoa wa Morogoro baada ya Mwili wake kufanyiwa uchunguz kwa zadi ya maaa 48.

Baada ya ibada fupi iliyofanyika kwenye hospitalini hapo kukamilika, wananchi waliofulika eneo hilo walipata fursa ya kutoa heshima zao za mwisho kwa marehemu na kabla ya safari ya kusafirisha mwili wa marehemu kueleka Moshi haijaanza.

Miongoni mwa watu walishiriki kwenye tukio hilo ni pamoja na viongozi wa jeshi la polisi, walioratibu kila kitu ikiwemo kutoa gari la kusafirishwamwili, waandishi wa habari, ndugu na jamaa wa marehemu.
Blogzamikoa
www.blogszamikoa.blogspot.com 

1 comment:

Anonymous said...

Baada ya kufanya uchunguzi jibu walilopata ni kajinyonga????? Pls rekebisheni maandishi ya hapo juu. Andikeni alie uwawa bado mnakuwa na uoga wa kusema ukweli dunia ya Leo?????.? Wanafanya unyama arafu mnawafichia Siri zao???? Tutaendelea lini?????. Kwani hamkosoma baruwa??? Picture alioninginizwa na kitanzi iangalieni vizuri then Kama mna akili mtajuwa kama alijinyonga au lah! Picture iko so clear hamnahaja ya Wana forensic science.