ANGALIA LIVE NEWS

Monday, December 3, 2012

KILIMANJARO STARS , ZANZIBAR ZATINGA NUSU FAINALI

Wachezaji wa Zanzibar wakiwa wamembeba kipa wao, Mwadini Ally baada ya kupangua mkwaju mmoja wa penalti, na kuiwezesha timu hiyo kutinga Nusu Fainali ya Kombe la Mataifa ya Afrika Mashariki na Kati, CECAFA Tusker Challenge baada ya kuifunga Burundi kwa penalti 5-4 kwenye Uwanja wa Lugogo, mjini Kampala, Uganda jioni hii. Zanzibar sasa itacheza na mshindi kati ya Kenya na Malawi.
KIKOSI cha Kilimanjaro Stras leo kimetinga hatua ya Nusu Fainali ya Michuano ya Chalenji inayoendelea nchini Uganda baada ya kuilaza bao 2-0 timu ya Rwanda 'Amavubi'. Bao la kwanza la Kili Stars limewekwa kimiani na Amri Kiemba dakika ya 33 ya mchezo baada ya kupokea pasi safi kutoka kwa Mwinyi Kazimoto wakati la pili likifungwa na mshambuliaji hatari, John Bocco dakika ya 54 ya mchezo akimalizia mpira uliotemwa na kipa wa Rwanda baada ya kushindwa kudaka shuti kali lililopigwa na Mwinyi Kazimoto. Kwa matokeo haya, Kili wanasubiri kucheza mchezo wa nusu fainali utakaopigwa siku ya Alhamisi Desemba 6 mwaka huu, wakati Amavubi wakiyaaga mashindano hayo.

No comments: