Advertisements

Thursday, January 3, 2013

YANGA KUIVAA ARMINIA BIELEFELD JUMAMOSI

Wachezaji wa Young Africans wakiwa mazoezini katika viwanja vya Fame Residence leo asubuhi

Timu ya Young Africans Sports Club yenye makao makuu yake jijini Dar es salaam nchini Tanzania siku ya jumamosi itashuka dimbani kucheza mchezo wa kirafiki na timu ya Arminia Bielefeld ya kutoka nchini Ujerumani, mchezo utakaofanyika katika mji wa Antalya.
Young Africans ambayo imeweka kambi ya mafunzo jijini Antalya itatumia mchezo huo kama fursa pekee ya kuweza kujipima uwezo dhidi ya timu hiyo ya Ujerumani ambayo pia imekuja kambi ya mafunzo kujiandaa na mzunguko wa ligi daraja la pili nchini Ujerumani.
Kocha Mkuu wa Young Africans Ernest Brandts amesema kwao ni furaha kwa kupata nafasi ya kucheza na timu kubwa kama ya Armini Bielefeld ambayo inawachezaji wa kiwango cha kimataifa hivyo anaamini utakua ni mchezo safi na kuwavutia.
Unajua tuna siku tano (5) tangu tufike hapa mjini Antalya Uturuki na tumeshafanya mazoezi kwa siku nne (4) hivyo fursa ya kupata mchezo wa kirafiki ni nzuri sana kwetu kwani itanipa nafasi ya kuona wachezaji wangu wameshayashika kwa kiasi gani mafunzo yangu alisema 'Brandts'
Haruna Niyonzima & Athumani Idd 'Chuji' wakiwa mazoezini leo asubuhi katika viwanja vya Fame Residence Football

Arminia Bielefeld imeshawasili mjini Antalya kwa ajili ya kambi yake ya mafunzo na hivyo kwao pia ni fursa nzuri ya kuweza kujipima uwezo na timu ya Young Africans ambao ni mabingwa mara 23 katika ligi kuu ya Tanzania.
Leo asubuhi Young Africans imeendelea na mazoezi katika viwanja wa Fame Residecne tayari kabisa kujiandaa na mchezo huo utakaochezwa siku ya jumamosi mjini Antalya.
Kikosi cha wachezaji 27 waliopo mjini Antalya wote wako katika hali nzuri na hakuna maheruhi hata mmoja hali itakayompa kocha Brandts kuamua kumtumia mchezaji yoyote katika mchezo huo.

Aidha kuhusu hali ya hewa leo jua linawaka toka asubuhi mpaka hivi sasa na kwa leo ni sentigred 23 mpaka 25, hivyo hali ya hewa ni nzuri kabis ana jua linawaka.

Wachezaji wakiendelea na mazoezi leo asubuhi

Wachezaji wa Young Africans wakiwa katika picha ya pamoja wakati wa mazoezi yao kwenye ufukwe wa Fame Residencxe, leo asubuhi.
Kikosi cha Young Africans Sports Club, kimeendelea na mazoezi yake leo katika uwanja wa Fame Residece Football uliopo Antalya na kisha jioni timu ikaenda kufanya mazoezi katika ufukwe wa bahari, eneo lililopo nyuma ya hoteli ya Fame Residence, ikiwa ni siku ya tatu katika ziara ya mafunzo nchini Uturuki kujiandaa na mzunguko wa pili wa ligi kuu ya Vodacom.
Kocha Mkuu wa klabu ya Yanga mholanzi, Ernie Brandts, amesema anafurahishwa na maendeleo ya kambi, kwani toka wameanza mazoezi jumatatu wakiwa nchini Uturuki ameona mabadiliko makubwa kwa wachezaji wake, huku akisema hofu iliyokuwepo kwa watanzania juu ya hali ya hewa ya baridi kali si kweli kwani hali ya hewa katika mjii huo ni ya baridi kiasi tu na hata leo katika mazoezi ya asubuhi palikuwa na jua la kawaida.
Wachezaji wanaendelea kuzoea mazingira, na kujifunza mambo mengi yanayohusu soka kwani wageni mbalimbali waliofika katika mji huo wamekuwa wakipenda kujua mengi kuhusiana na timu ya Young Africans na soka la Tanzania kwa ujumla.
Wachezaji wakiwa mazoezini Ufukweni Majira ya saa 10 kamili jioni kwa saa za Afrika Mashariki, timu ilifanya mazoezi ya ufukweni katika ufukwle wa Hotelu ya Fame Residence pemebezoni mwa Bahari ya Mediteranian.
Kocha wa makipa wa timu ya Bayern Leverkusen, Detier Gansi, jioni alishuhudia Young Africans ikifanya mazoezi ya ufukweni ambapo alisema amefurahia kuifahamu timu ya Yanga na wachezaji wake wanaonekana kuwa na morali ya kucheza soka, hivyo anaamini ziara hiyo itaisaidia timu kuwa pamoja na kujiandaa vyema na ligi alisema.
Wachezaji wakiwa katika mazoezi ya asubuhi uwanja wa Fame Residence Footbal.
Wakati huo huo mchezaji wa kimataifa wa timu ya Taifa ya Rwanda Haruna Niyonzima, amewasili jana jioni kwa ajili ya kuungana na wenzake kufuatia kuchelewa kuunganisha ndege siku ya jumamosi usiku akitokea nchini Rwanda alipokuwa amekwenda kuichezea timu yake ya Taifa.
Habari na Picha kwa hisani ya www.youngafricans.com

No comments: