Thursday, February 21, 2013

Q-CHIEF AMJIBU DIAMOND, ‘HE IS A GOOD KID, I LOVE HIS MUSIC, SIAMINI KATIKA UCHAWI’


Baada ya jana Diamond Platnumz kufunguka kwa undani jinsi anavyochukizwa na kitendo cha mwanamuziki mwenzie Abubakar Katwila aka Q-Chief kumsema anatembelea nyota yake, Q-Chief amezungumza na Bongo5 kujibu shutuma hizo.
Katika kipindi cha XXL cha Clouds FM jana, Diamond alisema, “mimi sipendezewi na anvyowaambia watu kuwa mimi namroga, kwa nini nisitembelee nyota ya watu kama akina Omary, akina Ben Pol. Alumbane na wakubwa wenzie akina Dully Sykes, mimi sitaki, namheshimu abishane na wakubwa wenzie, mimi mdogo aniache na wadogo wenzangu.”

Akijibu shutuma hizo, Q-Chief amesema:
“Sijui wakati anajibu hayo maswali alikuwa kwenye hali gani, sijui alikuwa amekasirika, sijui alikuwa 'out of mood' sijui alikuwa okay, lakini 'all in all' najua kila mtu ana uhuru wa kuongea kile anachojisikia na hajawekea mipaka, as long as kina-msatisfy yeye na kinawafurahisha wengine kwenye umma.

Mimi watu wangu wamenichukulia positive hili jambo baada ya kusikikiliza walinirekodia nikasikiliza lakini 'am not a big fan of superstition so' siamini hivyo vitu lakini kitu ambacho naweza kusema huu najua ni mchezo mchafu na acha niucheze kwa hisia kwa sababu sijui huko mbele ni kitu gani kitakuja kunisaidia katika maisha na kunyamaza pia wakubwa wanasema ni ustaarabu. He is a good kid, I love his music, he is doing good.”

Pia Q-Chief ambaye wiki iliyopita aliachia wimbo mpya uitwa Akuro amesema atafurahi kumuona Diamond anakuja kwenye show yake ya kwanza tangu miaka mitano iliyopita itakayofanyika kwenye ukumbi wa New Maisha Club, Jumapili ya Februari 24.

“Ningependa awepo kwenye hii show aangalie kwa sababu mimi pia nimekuwa nikihudhuria na nimeshawahi kufanya show ya Diamonds are Forever naye aliniita kwa mapenzi yake and with open-hearted I did a good show,” amesema Q.
GPL

No comments: