Advertisements

Thursday, April 4, 2013

HEKA HEKA ZA USAFIRI JIJINI DAR BAADA YA SUMATRA KUTANGAZA NAULI MPYA

Kutokana na umamuzi wa Mamlaka ya Udhibiti Usafiri wa Nchi Kavu na Majini (SUMATRA) kupandisha nauli za usafiri wa mabasi,treni na gharama za bandari zitakazoanza kutumika April 12 mwaka huu, usafiri wa daladala jijini umeanza kuonekana wa shida, hasa nyakati za jioni ,kwani baadhi ya wenye mabasi ya daladala jijini Dar es Salaam wameanza kutumia mwanya huo na kuongeza nauli kinyemela hivyo kusababisha wananchi kutaabika na kusongama katika vituo vya usafiri
Barabara ya Jangwani, wakazi wa jijini Dar es Salaam, wakitembea kwa miguu.
Baadhi ya wanachi katika maeneo ya Jangwani jana wakitembea kwa miguu.baada ya kuona tatizo la kususbiri usafiri .
Tabu ya usafiri bararabara ya muhimbili, Baadhi ya wakazi jijini Dar es Salaam jana wakisubiri usafiri katika maeneo ya shule ya Sekondari ya Azania. 
Picha kwa hisani ya Sufiani Mafoto Blog na Mwanakombo Mbwana Omari Jumaa

No comments: