Sunday, May 19, 2013

MASUMBWI NA MPIRA:TASWA YAIBAMIZA TIMU YA NGUMI 2-1

Wanamasumbwi leo kwa uchache walijikusanya katika viwanja vya leaders na kukipiga mechi ya kirafiki ya kudumisha uhusiano mzuri baina yao. mechi hiyo ambayo iliandaliwa kimzaha huku baadhia ya wanamasumbwi wakiwa hawana taarifa ya mchezo huo walikurupuana asubuhi na kucheza mechi hiyo bila wasiwasi kana kwamba mpira wanaujua. walikuwa waandishi ndio walioanza kuliona lango la mabondia dakika za mwanzo za mchezo kupitia kwa majuto omar aliyepiga shuti kali la mbali ambalo lilimshinda bondia chipukizi issa omar na kuwa goli,huku wakicheza bila kujitambua mabondia walionesha uhai pale alipotoka paquiao na kuingia jose mbowe ambae aliwasumbua kimpira na kufunga goli kwa upande wa mabondia.
kipindi cha pili timu zote zilijipanga vizuri na hazikuweza kufungana huku mpira ukiiisha mabondia wakiwa bado apo fiti wakihitaji kuendelea na waandishi wakionekana wapo hoi kwa mikiki ya uwanjani.timu hizo zimepanga yafanyike marudiano zote zikiwa kamili.YAWEZA KUWA MECHI YA KUCHANGIA KITUO CHA MICHEZO YA NDANI (indoor)
Alphonce mchumia tumbo akiwa chini ya ulinzi wa mabaki wa taswa.
Francis Miyeyusho anajiandaa kutoka na nafasi yake ikachukuliwa na mashali.

ibrahim'bigright akitoa maelezo kwa timu ya mabondia huku thomas mashali akisikiliza kwa makini kabla ya kuingia.
majuto omari wa taswa na jimwili lake kashindwa kabisa kufurukuta kwa daudi muhunzi.majuto ndie aliefunga bao la pili la taswa.hapa kabla hajatulizwa kibondia.
Juu na chini ni timu ya mabondia ikipata mawaiza.
 Kikosi cha Taswa Fc, TIMU ya Taswa Fc jana iliibuka na ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya timu ya Full Mabondia, inayoundwa na mabondia mahiri wa Jijini Dar es Salaam. Timu hizo zilikutana katika mchezo wa kirafiki uliochezwa kwenye Viwanja vya Leaders Club, Kinondoni jijini Dar jana mchana, huku timu ya mabondia ikiwakilishwa na mabondia kama, Thomas Mashali, Mchumiatumbo, Francis Miyeyusho, Majia, Kanda Kabongo, na wengine wengi. Picha zote na www.sufianimafoto.com
 Wadhamini wa timu ya Taswa, Kampuni ya TSN, pia walikuwepo viwanjani hapo wakionyesha kinywaji cha Chilly Willy, kinachotengezwa na kampuni hiyo. Pichani ni baadhi ya warembo wanaotangaza bidhaa za kampuni hiyo, wakiwa katika meza yao.
 Beki wa Taswa Fc, Juma Ramadhan, (nyuma) akimdhibiti mshambuliaji wa Full Mabondia, wakati wa mchezo huo.
kwa picha zaidi bofya read more
 Beki wa Taswa Fc, Muhidin Sufiani 'Sufianimafoto' (kulia) akimfinya mchezaji wa Full Mabondia, wakati wa mchezo huo jana.
 Beki wa Taswa Fc, Elius Kambili, akiambaa na mpira.
 Beki wa Taswa Fc, Salim (kulia) akiondosha moja ya hatari mbele ya Bondia, Mchumiatumbo.
 Kipa wa Full Mabondia, akiwa golini huku akiwa peku peku, wakati wa mtanange huo jana.
 Zahoro Milanzi wa Taswa Fc, (kushoto) akiambaa na mpira wakati wa mtanange huo.
 Wachezaji wa Taswa Fc, wakipasha kabla ya kuanza kwa mtanange huo jana.
Sufianimafoto (katikati) akipozi na Bondia Francis Miyeyusho (kushoto) na 'Chuji' (kulia) kabla ya kuanza kwa mtanange huo jana.
Benchi la Taswa Fc.

No comments: