Monday, May 20, 2013

Spika wa bunge aliahirisha bunge kwa dharura kujadili hotuba ya kambi ya upinzani.

Spika wa bunge Mh. Anne Makinda ameliahirisha bunge kwa dharura kupisha kamati ya kudumu ya kanuni za bunge kukutana kwa ajili ya kuijadili hotuba ya kambi rasmi ya upinzani iliyokuwa ikisomwa bungeni kwa madai ya kuwa na baadhi ya maneno ya uchochezi na baadae kutoa maamuzi ya kuondolewa kwa maneno yote yaliyoko katika ukurasa wa kwanza hadi 14 wa hotuba hiyo

1 comment:

Anonymous said...

Mbona huo ni ukweli mtupu na kila mtanzania anafahamu kuwa serikali inahusika katika utesaji wa waandishi wa habari. Hayo siyo maneno ya kuudhi, ulimwengu mzima unafahamu kuwa hakuna uhuru wa habari,Je David Mwangosi alijiua mwenyewe? Je Saed Kubenea alijimwagia tindikali mwenyewe? Watanzania tuzinduke, hii nchi siyo ya chama cha mapinduzi wala siyo ya serikali. Tunataka haki itendeke kwa wale walioumua Mr. Mwangosi ambao ni polisi(Mkuu wa polisi wa mkoa awajibishwe) na watesaji wa Ulimboka na Kibanda (mbona wanafahamika ni usalama wa Taifa) washitakiwe bila hivyo nchi itabaki ya visasi.