Advertisements

Sunday, July 28, 2013

HASHEEM THABEET AIBUKIA NDANI YA BONGO STAR SEARCH

Mtanzania pekee anayeiwakilisha Tanzania kwenye ligi ya mpira wa kikapu nchini Marekani maarufu kama NBA, Hasheem Thabeet. Hivi karibuni alijunga na majaji wa Bongo Star Search kwa lengo la kuwapa moyo vijana ambao wanajaribu kuonyesha vipaji vyao kwenye shindano hili. Hasheem Thabeet ni moja ya vijana ambao wamefanikiwa kutumia vema vipaji vyao na kuwa mfano mzuri kwa vijana wengine kufanya juhudi kwenye talent zao.
Jaji mkuu wa BSS Rita Paulsen aliandika kupitia ukurasa wake wa facebook kwamba, “Rafiki yangu Hasheem Thabeet alikuja kuwapa moyo na kuonyesha support yake kwa vijana wanaofanya usaili. Namshukuru sana kwa mchango wake”.

1 comment:

Anonymous said...

hasheem mdogo wangu pamoja na kukupenda sana na ningependa sana uendelee na ukuze kipaji chako cha basketball, lakini sidhani kama safari yako katika NBA ina muda mrefu. naona umeshachoka na challenge za NBA na timu karibu zitaonesha kuchoshwa nawewe. bora hata uanze mazoezi ya kuimba Taarabu pengine utafanya vizuri zaidi.