Lengo:
Hili ni jukwaa ambapo wataalamu, wakereketwa na wafurukutwa wa Kiswahili - kupitia Chama cha Ukuzaji wa Kiswahili Duniani (chaUKIDU: www.chaukidu.org ) chenye makao makuu yake nchini Marekani – wanakuleteeni makala au mijadala mifupi ya uchokonozi kuhusu masuala anuai ya Kiswahili kama vile ukuaji wa msamiati, aina za msamiati, mikanganyiko na mikengeuko ya kisarufi na hata ya kitahajia, miktadha ya mawasiliano na athari zake katika matumizi ya lugha, sera za lugha, Kiswanglish, nk. nk. Lengo ni kuwa na jukwaa shirikishi katika ukuzaji na uendelezaji wa lugha yetu pendwa. Jivunie Kiswahili
Kuna Kiswahili
kimoja au Viswahili vingi?
Liliibuliwa ama liliibuka suala la ‘usahihi’ wa lugha: ni
Kiswahili kipi ni sahihi na kipi sio sahihi! Mintaarafu hoja hii, nimevutiwa na
kamusi hizi mbili zilizotungwa na taasisi mbili tofauti katika Jamhuri ya Mungano
wa Tanzania zinazoshughulikia taaluma ya Kiswahili, BAKIZA na TUKI (sasa
TATAKI). Ni taasisi ipi iko sahihi kuhusu neno ‘kamusi’? Baraza la Kiswahili la
Zanzibar (BAKIZA) linakiita kitabu chake Kamusi
la Kiswahili Fasaha (Oxford, 2010)na Taasisi ya Uchunguzi wa Kiswahili
(TUKI) inakiita kitabu chake Kamusi ya
Kiswahili Sanifu (Oxford, 2004). Kwa mujibu wa BAKIZA kuna ‘kamusi’ (li-) na ‘makamusi’ (ya-) na kwa mujibu wa
TUKI, kuna ‘kamusi’ (i-)/(zi-). Lakini
pia vitabu hivi vinaibua dhana ya ‘Kiswahili Sanifu’ na “Kiswahili Fasaha’. Kwa
maoni yangu, ‘kamusi la Kiswahili’ ni Kiswahili fasaha na ‘kamusi ya Kiswahili’
ni Kiswahili sanifu. (Charles Bwenge, cbwenge@ufl.edu
)
No comments:
Post a Comment