Kutoka makavazini:
“Tukitoe Kiswahili utumwani kwanza”
Katika toleo la gazeti la RAI la Agosti 11-17, 2005 Ndugu Prudence Karugendo aliandika makala
nzuri iliyobeba kichwa cha habari “Tukitoe Kiswahili utumwani kwanza”. Mojawapo
ya hoja zake ilisomeka hivi:
Kuazima,
kukopa na kutohoa (kupora) maneno ya Kizungu na Kiarabu na kuyaingiza katika
msamiati wa Kiswahili nakupinga kwa sababu zifuatazo: Kwanza, ni kudhoofisha
Kiswahili kwa kukiwekea viraka, jambo linalokifanya kionekane kama lugha isiyo
na msamiati unaojitosheleza. Pili, kunakiondolea uasili wake na kukipotezea
maana mahususi ya ujumbe unaobebwa na lugha, yaani kueleza kwa watumiaji wapya
mila na desturi za watu wa asili ya lugha husika. Tatu, hili neno ‘kutohoa’
naweza nikalitafsiri kama kupora. Kwa vile hakuna makubaliano yanayofanyika
kati ya lugha mbili ili kuamisha neno kutoka lugha moja kwenda lugha nyingine.
Basi kutohoa neno au maneno ni kupora maneno ya lugha moja na kuyapachika
katika lugha nyingine. Hivi kweli hili ni jambo la kujivunia na kuzunguka dunia
kunadi lugha iliyojaa maneno yaliyoporwa? Kwa maana hiyo kutohoa maneno na
kuyajaza kwenye Kiswahili chetu hakutufai.”
Maoni yangu:
Katika zama hizi za
utandawazi, dhana mpya zinaingia kila siku na kwa kasi kubwa katika jamii ya
wazungumzaji wa Kiswahili. Kila dhana mpya inapoingia huhitaji kupewa jina ili
kuwezesha mawasiliano. Kukopa na kutohoa ni mojawapo ya njia mujarabu za kuziba
mapengo hayo ya kimsamiati. Hata hivyo, utohozi unaweza kudhoofisha lugha iwapo
unatumiwa vibaya. Katika tangazo hili bainisha utohozi mzuri na mbaya na toa
sababu. (cbwenge@ufl.edu )
"pata intaneti na bado muda wa maongezi kwa miezi sita bure"
No comments:
Post a Comment