Thursday, November 21, 2013

AIBU NOMA..! INAWEZA KUKUKOSESHA MAMBO YA MAANA WAKATI WOWOTE SOMA HAPA MBINU ZA KUIEPUKA

WATU wenye aibu ndani yao wanafahamu fika kuwa kuna mambo mazuri yanawapita lakini wanahisi hawana jinsi ya kubadilisha hali hiyo.
Aibu kimahesabu ni sawa na:
AIBU = KUKOSA FURSA + KUKOSA FURAHA + KUFAHAMIANA NA WATU WACHACHE
Aibu ni kizuizi kikubwa sana kwa mwenye nayo kufikia mambo mazuri katika jamii.
Lakini naomba nikuambie hata kama wewe ni mmoja wao kuanzia leo 
unaweza kubadilisha hali hiyo kwa kutumia hatua zifuatazo:
1.MTAZAMO WAKO JUU YA WATU WENGINE
Watu wenye aibu mara nyingi wanajaribu kujitofautisha na 
watu wapya wanaokutana nao na kuwapa hadhi inayowazidi wao.
Hali hiyo itakufanya ujione huna jipya la kumueleza au kuzungumza mbele ya watu hao.
Unachopaswa kufanya ni 
kumuona kila mtu mpya unayekutana naye kama wa kawaida na hana alichokuzidi na kwamba hata yeye kuna vitu hajui 
au hana ambavyo wewe unavyo.
2.TAMBUA HATA WENGINE WANA AIBU PIA
Usijiweke peke yako kama ndio mtu mwenye aibu kupita wote na kwamba wengine 
hawako kama wewe.
Kuanzia leo tambua kuwa kila mtu ameumbwa na aibu ndani yake pale anapokutana na mtu mpya kwahiyo ukiwa 
mbele ya watu wapya 
jua hata wao pia wanakuonea aibu kwa kuwa hawajui ulichonacho ni nini.
3.KUSANYA TAARIFA NYINGI KICHWANI
Mtu mwenye aibu siku zote hujiona hana chochote cha maana 
kuwashirikisha wengine.
Kuna wengine wanakuwa kweli hawana vitu vya kuzungumza mbele za watu wengine na kuna wengine ni 
kujidharau tu na kuona taarifa walizo nazo hazina maana.
Jaribu kuwa na tabia ya kusoma vitu vipya na kuwaeleza watu wengine 
na hapo utafanya uwezo wako wa kusimama au kujitokeza mbele ya watu wengine kuwa mkubwa kwa kuwa kichwani 
una kitu cha kuwashirikisha.
4.ONGEZA KUJIKUBALI
Ukiwa na tabia ya kujidharau mwenyewe na kujiona huna thamani 
mbele ya wengine utafanya aibu ikuteke 
daima.
Thamini uwezo wa pekee 
ulionao na upe thamani kuwa hakuna mwengine alionao kwahiyo hata wewe 
unaweza kuwaonyesha maajabu wasiyoyajua.
Ukijiweka katika kundi 
hili hautakuwa muoga wa kuwasiliana 
na watu wapya kila siku.
5.ACHA KUZIAMINI HISIA HASI
Mtu mwenye hofu siku zote anatengeneza hisia ndani yake kuwa baada
ya yeye kufanya au kusema jambo fulani
basi watu wengine watafanya
kitu fulani kwake.
Mathalani anaweza akaanza kuhisi kuwa baada ya yeye kukosea kitu 
watu watamcheka au kumsema vibaya
kwa wengine.
Na anapoiamini hiyo picha kichwani kwake anaongeza aibu na kushindwa kuitumia fursa iliyopo mbele yake.
Na mara nyingi hizi hisia huwa hazina ukweli wowote katika matukio
halisi ila ni hofu tu anayojijengea mwenyewe.
Anza kujitengenezea hisia chanya kuwa watu watakupongeza kwa kujaribu.


KUNA MSEMO USEMAO: 
"AIBU YAKO NDIO UMASIKINI WAKO"
HAINA UBISHI UKIENDEKEZA TABIA YA KUONA AIBU MBELE ZA WATU KAMWE HAKUNA FURSA UTAKAYOPATA.


TAMBUA PIA: "MAFANIKIO YA MTU YAPO MIKONONI MWA MTU"
NI KUPITIA BINADAMU WENZETU NDIO TUNAFIKIA NDOTO NA MAFANIKIO KATIKA MAISHA YETU HIVYO USIIACHE AIBU IKUTENGE NA NDOTO YAKO.

No comments: