Sehemu ya wanajeshi wanaouhudumu katika Misheni ya Umoja wa Afrika ( AMISOM) wakiwa katika majukumu yao ya kulinda amani nchi Somalia. Misheni hiyo imeongezewa uwezo wa muda na Baraza Kuu la Usalama wa Umoja wa Mataifa, katika mkutano wake uliofanyika siku ya jumanne uwezo huo ni pamoja na kuongeza idadi wa wanajeshi zaidi ya 4,000, upelekezaji wa helkopta pamona na vifaa vingine lengo likiwa kuiwezesha misheni hiyo kukabiliana vilivyo na vitisho vya wapiganaji wa Al-Shabaab
Katika
kuhakikisha kwamba Misheni ya Umoja wa
Afrika inakabiliana vilivvo na kundi la
wapiganaji la Al-Shabaab, Baraza kuu la
Usalama la Umoja wa Mataifa, jana
jumanne ,limepitisha kwa kauli moja Azimio
linaiongezea uwezo muda Misheni
hiyo.
Kupitia
Azimio hilo Misheni ya Umoja
wa Afrika katika Somalia kwa kifupi kama AMISOM inaongezwa
wanajeshi zaidi ya 4, 000 pamoja na misaada ya vifaa ili iwe na
uwezo mkubwa wa kukabiliana
vilivyo na ongezeko la vitisho kutoka
Al-Shabaab.
Aidha Azimio
hilo ambalo lilipitishwa kwa kauli moja na wajumbe 15 wanaounda Baraza
Kuu la Usalama, pia limeongeza
muda wa mamlaka ya misheni hiyo hadi
Octoba 31, 2014. Misheni ya Umoja wa Afrika ya kulinda amani nchini Somalia iliundwa mwaka 2007
Azimio hilo
pia linaiomba Umoja wa Afrika
kuongeza nguvu ya jeshi hilo kwa maana
ya kuongeza wanajeshi Zaidi
kutoka 17,731 waliopo sasa hadi kufikia
22, 126, na pia limeazimia kupanua misaada yake ya kilojistiki inayotolewa na Umoja wa Mataifa kwa Misheni
hiyo .
Aidha Baraza Kuu la Usalama kupitia azimio hilo, linasisitiza
kwamba, uamuzi huo wa kuiongezea
nguvu Misheni ya Umoja wa Afrika unalenga katika kuimarisha uwezo wa kijeshi wa
AMISOM katika kipindi cha miezi 18 hadi 21 na kwamba baada ya kipindi hicho tathimini itafanyika kuangalia kama
kutakuwa na haja ya kupunguza nguvu ya
Misheni hiyo.
Taarifa Zaidi zinaeleza kwamba Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa na Umoja wa
Afrika hivi karibuni kwa pamoja walipendekeza
kuimarishwa kwa Misheni hiyo ya AMISOM ikiwa ni pamoja na kupelekewa helkopta na
zana nyinginezo, kwa lengo la kukabiliana na vitisho vya aina yoyote katika pembe ya Afrika.
Vilevile
kupitia Azimio hilo Baraza Kuu la Usalama pia
limepokea taarifa kuhusu pendekezo
la Katibu Mkuu
wa Umoja wa Mataifa la kutaka kupeleka
kikosi maalum cha kulinda majengo
yaUmoja wa Mataifa nchini Somalia (UNSOM)
ambayo ilianzishwa mweji Juni kwa
lengo la
kuisaidia Serikali na wananchi wa Somalia katika juhudi zao za kuleta usalama
na ustawi.
Baraza pia limetoa wito wa kuongezea ushirikiano kati ya AU, Umoja wa
Mataifa na Serikali ya Shirikisho ya Somalia, ikiwa ni pamoja na utekelezaji wa mpango
mpana wa amani, usalama na maendeleo.

No comments:
Post a Comment