Advertisements

Thursday, November 21, 2013

KAKA,….DAWA KWA KIPIMO IKIZIDI SUMU

LEO nitatoka kimjini zaidi kwa kuwasalimi mambo? Yangu hali buheri wa afya njema kwa uwezo wake Manani. Kama ilivyo ada tumekutana kwenye kona yetu ambayo hukutia muwashawasha kiti hakikaliki mtoto wa kike tatizo nini. Unajua kuna kitu kinachekesha kuna watu wamenitumia ujumbe wa simu kwa vile ukipiga simu nisiyoijua huwa sipokei.

Eti anti Na tunataka tukuone live, mnione live ili iweje? Mimi nafikiri hiki nikisemacho ni muhimu kuliko sura yangu, sasa hivi natisha uso kama nyani mzee. Mwingine Ooh! Anti Na, nataka mchezo na wewe eti yupo tayari hata kunihonga gari kwa vile tu nimeonekana mapenzi nayajua.

Hujakosea mpaka kuwa nyani mzee basi nalijua pori lilivyo, kwa hiyo mapenzi nayajua haswaaa. Sasa wewe unanitaka ili upate raha ya mapenzi au unikomoe? Vijana wa kileo ambao kila kukicha mnatangaziwa dawa mpya ya kuongeza ukubwa wa maumbile, nikupe ili iweje? Kisa cha kunilaza kitandani mwezi mzima kama nimedondoka kwenye mnazi.Jamani mapenzi starehe ukikutana na mwanaume akiondoka lazima hamu zikujie, siyo ukikutana na mwanaume ukimbie na kufuli mkononi, nani aliyekwambia mapenzi vita au kwa vile nimekunywea pombe yako na vikuku vyako?
Wanaume bwana, ukimlia vyake mpaka mnaachana chini panakuwaka moto kama ulikuwa unachochewa na kuni kuchemsha mawe.

Hakaa babu wee, mapenzi ukiyajua wala hutumii nguvu muandae mwenzio basii wewe taratibu unapiga pederi wala hutumii nguvu na mwenzako maneno yote yanamwisha mdomoni kwa raha ya safari, siyo mwenzio anauma memo mwanzo mwisho kama anataka kujifungua. Jamani nataka kuwaeleza vijana wa kileo kuwa na bakora kubwa si uanaume au ndiyo kumfurahisha mwanamke.

Nataka leo niwaibie siri kuwa wanawake wengine wamekaa kwenye ndoa zao wafanye nini. Mwanaume kama kaficha mguu wa mtoto na akipanda juu ya mnazi hajui hata chenga yeye mbele kama faru. Jamani mwanaume anatakiwa kutumia mtindo unaulingana na maumbile yake, Siyo kupiga pederi na kumwaga mzigo bila kujua mwenzako anafurahi au vipi?

Jamani mtaona natania kuna msichana mmoja kaikataa ndoa baada ya kukutana na bakora mujarabu, mwanaume alikuwa manshallaah! Mungu alimjalia wala hakuongeza kwa waganga alikuwa na maumbile ya kuzaliwa. Kibaya zaidi mwanaume wake akipanda amepanda hateremki baada ya saa mbili. Mtoto wa kike kila siku ugonjwa wa tumbo haumuishi.

Kavumilia yakamshinda kila akirudi kwao analazimishwa kurudi, amevumilia miezi minne mtoto katoroka alipokwenda hapajulikani. Basi nataka kuwaeleza waume zetu pamoja na kuzifuata bakora ambazo hatuwezi kupewa na baba zetu basi mtupe raha si karaha. Jamani, ukiona mwanamke anabana mapaja au anakusukuma ujue unamuumiza hapo hakuna mapenzi bali mateso.

Kuwa na bakora mujarabu si dhambi bali ujue basi kipimo unachotakiwa kumpa mwenzako. Ukiwa umejaliwa basi mpe mwenzio kama dozi ya dawa, kuna kipimo cha mm 5 wewe unampa mm 20 huoni kama unataka kumuua kwa kuzidisha dozi. Sasa hivi watoto wengi wa kike wamekuwa na matatizo ya tumbo kutokana na waume zao kuwatumia vibaya matokeo yake mimba hakuna na chango kila kukicha. Hebu jamani tubadilike si wanaume wote waliokwenda hospitali na kuvalishwa pete.

Wasiokwenda wamekuwa tatizo katika ndoa zao kwa kuamini wake zao wana matatizo kumbe tatizo ni wao wenyewe kuzidisha dozi na kugeuka sumu.
Sungura anaweza kumbeba tembo kwa mipango siyo nguvu, tumieni mitindo ya mapenzi kuwapa raha wapenzi wenu.Leo naishia hapa ila wiki ijayo mtakuwa na babu poa kuwafunda wanaume matumizi ya mitindo ya mapenzi ili kumpa raha mwenzako.
Ni mimi Anti Nasra

No comments: