ANGALIA LIVE NEWS

Thursday, November 14, 2013

MISS ARUSHA 2001 AOLEWA NA MJESHI WA KIMAREKANI.

Sharon Pownall akiwa na mumewe Dylan. Tukio hilo lililogusa hisia za watu wengi lilitokea hivi karibuni mjini hapa, lilifanyika katika Ukumbi wa Hoteli ya Ngurudoto na kuhudhuriwa na mamia ya watu.Kwa mujibu wa chanzo makini kilichohudhuria harusi hiyo iliyofungwa kanisani, kulikuwa na kikundi cha watu ambacho hakikupenda kuona miss huyo akiolewa kiliisengenya ndoa hiyo.
...Wanandoa hao wakishuka ngazi wakati wa ndoa yao.
“Kuna kikundi cha watu kilikuwa hakipendi kuona Sharon anaolewa hivyo kilikuwa kikipambana chinichini kuhakikisha ndoa hiyo haifungwi lakini bahati mbaya kimeshindwa,” kilisema chanzo hicho.
Bibi harusi Sharon.
Hata hivyo, pamoja na kampeni hizo za kuvuruga ndoa hiyo, kwa upande wake Sharon alimshukuru Mungu kwa kufanikisha ndoa hiyo aliyokuwa akiisubiri kwa hamu.
“Namshukuru Mungu kwa kuwa kila kitu kimekwenda vizuri na sasa nimekuwa mke kamili wa ndoa, kama kuna mtu alikuwa na kijiba cha roho atabaki nacho milele,” alisema miss huyo.
Bwana harusi Dylan

No comments: