*KUCHANGIA KATIKA KUKABILIAN A NA MABADILIKO YA HALI YA HEWA
*WATAANZIA NA NCHI ZA TANZANIA NA MALAWI.
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Hali
ya Hewa Dkt. Agnes Kijazi na Mkurugenzi wa utafiti Dkt. Ladislaus Chang’a walishiriki
katika hafla fupi ya kusaini makubaliano hayo kati ya Shirika la Hali ya Hewa Duniani
na Serikali ya Norway yaliyofanyika mjini Warsaw Nyumbani kwa Balozi wa Norway
nchini Poland tarehe 21 Novemba,2013.
Kutoka
kushoto ni Katibu mkuu wa Shirika la Hali ya Hewa Duniani (WMO) Bw.Michel
Jarraud, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe; Dkt. Jakaya Mrisho
Kikwete, Msaidizi wa Katibu mkuu wa Shirika la Hali ya Hewa Duniani (WMO) Bi.
Elena Manaenkova na kulia kabisa ni Mkurugenzi
Mkuu wa Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) Dkt. Agnes Kijazi katika mkutano
wa COP 19 huko Warsaw Poland
Katibu
Mkuu wa Shirika la Hali ya Hewa Duniani alipomtembelea Mheshimiwa Rais katika
hoteli ya Bristol tarehe 20 Novemba 2013, alimjulisha kuhusu msaada huo na
kwamba Tanzania imechaguliwa kuwa nchi ya awali katika kutekeleza mpango huo
kwa imani kwamba TMA itasimamia vyema utekelezaji wake na kupata matokeo mazuri
yatakayosaidia kupanuliwa kwa mpango huo katika nchi zingine za Afrika. Kwa
upande wake Mheshimiwa Rais alimshukuru Bw. Jarraud kwa misaada ambayo WMO
inaisaidia Tanzania na aliahidi kwamba serikali itaendelea kuisaidia Mamlaka ya
Hali ya Hewa ili iweze kutekeleza majukumu yake na kushiriki vyema katika
program za WMO.
No comments:
Post a Comment