Wawakilishi wa Kudumu kutoka nchi 193 wanaoziwakilisha nchi zao katika Umoja wa Mataifa, wakimsikiliza Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Ban Ki Moon wakati alipolizungumza Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa siku ya Ijumaa. Alitumia fursa hiyo, kuainisha vipaumbele vyake vya mwaka 2014, mafanikio na changamoto zinazoukabili Umoja wa Mataifa ikiwamo migogoro inayoendelea huko Sudan ya Kusini, Jamhuri ya Afrika ya Kati na kwingineko Duniani. Akatahadharisha kwamba kama Jumuiya ya Kimataifa haitakuwa makini kuna hatari kubwa ya kutokea mauaji makubwa ya raia kama ambavyo imeshawahi kutokea huko nyuma.
Na Mwandishi
Maalum
Kufuatia
machafuko na migogoro
inayoendelea katika nchi za Sudani ya
Kusini, Afrika ya
Kati , Mali na maeneo mengine
duniani, Katibu Mkuu wa Umoja wa
Mataifa ameitaka jumuiya ya kimataifa
kuwa makini na kuchukua tahadhari
ya juu.
Amesema kuna
ukiukwaji mkubwa wa haki za binadamu katika maeneo hayo jambo
analosema hali ikiendelea kama ilivyo sasa kuna
hatari kubwa ya kutokea mauaji makubwa ya raia kama ambavyo dunia imeshuhudia katika miaka iliyopita.
Ban Ki Moon, ametoa tahadhari hiyo, mwishoni mwa
wiki, wakati alipolizunguza Baraza Kuu
la Umoja wa Mataifa . Ambapo alitumia fursa hiyo kuainisha malengo
na vipaumbele vyake na Umoja wa Mataifa kwa ujumla kwa mwaka huu wa
2014.
“Kuna mambo ambayo
tunapashwa kuwa makini nayo na kuchukua tahadhari kubwa, mgogoro unaoendelea katika Sudan ya Kusini umefikia
kuwango cha kutisha. Kuna
ukiukwaji mkubwa wa haki za
binadamu “ akasema Ban Ki Moon
Na kuongeza kwamba
kufuatia mgogoro huo Umoja wa Mataifa ulifungua
milango ya Kambi ya Kulinda Amani katika Sudan ya Kusini ( UNMISS) na
kuwahifadhi maelfu ya raia waliokuwa katika hatari kubwa ya kupoteza maisha
yao.
“ Wengi wao leo hii
wako hai ni kwasababu tu, waliwahi kukimbia kwa wakati na kufika kwenye
makambi yetu. Tunajitahidi kadri tuwezavyo pamoja na uwezo wetu mdogo
kuwa hudumia, lakini hali ni mbaya na mazingira ni ya kutisha” akasisitiza.
Pamoja na
kuendelea na jukumu la utoaji wa misaada kwa raia ambao
wameyakimbia makazi yao, Mkuu huyo wa
Umoja wa mataifa anaeleza kwamba, jitihada za kutafutu suluhu ya kisiasa kwa
mgogogo huo inaendelea.
Akatumia fursa hiyo
kuwashukuru viongozi wa nchi za IGAD (
Intergovernmental Authority for Development ) na Umoja wa Afrika ( AU) kwa juhudi zao za kusimamia mazungumzo ya
kutafuta suluhu.
Aidha katibu Mkuu amezitaka pande zinazohusika kumaliza tofauti zao kwa njia ya
mazugumzo na kuonya kwamba Ofisi ya Kamishna
ya Haki za Bindamu inafuatilia kwa karibu sana kuhusu ukiukwaji wa haki
za binadamu katika nchi hiyo .
Kwa upande wa Jamhuri
ya Afrika ya Kati, Mkuu huyo wa Umoja wa
Mataifa, ameelezea wasiwasi wake kuhusu
mwenendo wa mambo unavyoendelea yakiwamo
mauaji holela ya raia.
Akazishukuru nchi zinazounda
Jumuiya ya Kiuchumi ya Mataifa ya Afrika ya Kati ( ECCAS) pamoja na Ufarasa kwa
juhudi zao za kuwasaidia raia wa nchi hiyo pamoja na kurejesha hali ya amani
na utulivu. Nakuonya kwamba wale wote wanaouhusika na ukiukwaji wa haki za
binadamu lazima watawajibishwa.
Kuhusu Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo ( DRC) Katibu Mkuu ameeleza kuwa uwepo wa Brigedi Maalum ( FIB) katika eneo la
Mashariki ya Nchi hiyo, kumesaidia sana
katika kuweka sawa mambo ikiwa ni pamoja
na kupunguza kujirudia kwa machafuko ya
mara kwa mara.
Akasisitiza kwamba Jumuiya ya Kimataifa inapashwa kutumia hali ya utulivu iliyopo hivi sasa
katika eneo hilo, kutekeleza Mpango
Mpana wa Umoja wa Mataifa kuhusu siasa, amani na maendeleo
katika DRC na Maziwa Makuu.
Pamoja na kuzungumza migogoro inayoendelea katika baadhi ya nchi
za Afrika, Mkuu huyo wa Umoja wa Mataifa
pia alielezea wasi wasi wake kuhusu
sintofahamu zinazoendelea katika
baadhi ya nchi za Asia na Ulaya
hususani muendelezo wa chuki na uhasama kwa kimsingi ya tofauti za
dini, na ukabila.
Akagusia pia
migogoro inayoendelea katika Mashariki ya Kati hususani katika nchi za Syria, Misri na mgogoro kati ya Israel na Palestina
Katika hatua
nyingine, Katibu Mkuu Ban Ki Moon, amesema Umoja wa Mataifa, haupashwi
kuziomba au kuzibembeleza nchi wanachama
pale unapohitaji kupatiwa
wanajeshi, polisi au vifaa
wakati ambapo raia wasiokuwa na hatia wakiendelea kuteseka na kupoteza
maisha.
Akasisitiza kwamba Umoja wa Mataifa ni chombo muhimu
ambapo maamuzi mengi yamekuwa yakifanyika lakini akasema anatiwa
shaka na baadhi ya misimamo ya
viongozi au nchi zenye ushawishi
mkubwa.
Pamoja na kuelezea matatizo ya kisiasa na kiusalama na
changamoto zake, pia aliainisha baadhi
ya mafanikio ya chombo hicho katika mwaka uliopita na kazi kubwa iliyombele
yake na hasa likiwamo jukumu ya utayarishaji wa malengo mapya ya maendeleo endelevu baada ya
mwaka 2015.

No comments:
Post a Comment