Waziri wa
Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais anayeshughulikia Mazingira, Dk. Binilith
Mahenge (Aliyevaa shati la drafti) akiwa na viongozi wa mkoa wa Iringa
na wa Manispaa ya Iringa.
Ujenzi wa
kituo cha Mabasi cha Igumbilo Manispaa ya Iringa umesitishwa baada ya
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais anayeshughulikia Mazingira, Dk.
Binilith Mahenge kuamuru tathimini ya athari ya mazingira ifanywe upya.
Waziri
amefikia uamuzi huo kufuatia kupata malalamiko juu ya athari za kujenga
kituo hicho kutoka kwa Wizara ya maji, Mkoa wa Iringa na Mamlaka ya maji
safi na maji taka mjini Iringa (IRUWASA) kuwa ujenzi wa kituo hicho
utaathiri afya za watumiaji wa maji wa Iringa.
Anasema ni vema Halmashauri ya Manispaa hiyo kusitisha shughuli zote za kuendeleza eneo hilo kusubiri maamuzi ya serikali.
Waziri Mahenge anasema hayo mara baada ya kupata taarifa juu ya maji mkoa na kutembelea eneo la ujenzi wa kituo hicho.
Anasema
kuwa hawezi kulitolea uamuzi suala la ujenzi wa kituo hicho bila
kuwashirikisha wataalamu na kumuagiza Mkurugenzi Mkuu wa Baraza la
Usimamizi wa Mazingira (NEMC), Bonaventura Baya kurudia kufanya
tathimini upya ili kubaini tatizo lilopo pamoja na madhara
yatakayojitokeza.
Naye
Mkurugenzi wa NEMC , Baya anasema watafanya tathimini hiyo kwa muda wa
wiki mbili na kuhakikisha kuwa majibu yatakuwa tayari ili kuweza
kusaidia maamuzi kutolewa mapema kwa kufuata ushauri wa wadau mbalimbali
juu ya ujenzi huo wa stendi ya Igumbilo.
Mstahiki Meya
wa Manispaa ya Iringa, Amani Mwamwindi anasema ni vema haki ikatendeka
ili jambo hilo lisichukuliwe na kuonekana ni suala lenye maslahi ya
kusiasa kwa baadhi ya wanasiasa.
Mkuu wa
Mkoa wa Iringa, Dk. Christine Ishengoma alisema kinachotakiwa ni kufanya
subira ya matokeo ya NEMC na maamuzi ya serikali na kuwa kujenga au
kutojenga kituo hicho ni maamuzi yatakayotolewa na serikali.
Akitoa
Taarifa kwa waziri, Katibu Tawala wa Mkoa, Wamoja Ayubu anasema kuwa
ujenzi wa kituo hicho ni mzuri na unadhana ya kuboresha miundombinu ya
Manispaa ya Iringa, kukuza uchumi pamoja na kuvutia wawekezaji.
Aidha
Wamoja anasema maji ya mto ruaha ni chanzo muhimu cha maji kwa wakazi wa
Manispaa ya Iringa na kuwa IRUWASA imewekeza zaidi ya Sh70 Bilioni
kwenye mto huo ili kuwapatia wananchi maji safi.
Iruwasa
wanadai kuwa ujenzi wa kituo hicho utaendanana na shughuli za kibiashara
na gereji jambo litakaloathiri maji kwa kuwa chujio zilizofungwa hazina
uwezo wa kuchuja tqaka kemikali.
Wamoja
alisema kuwa ujenzi huo endapo utatiririsha maji machafu taka ngumu na
kemikali itaathiri maji ya mto Ruaha na pia itasababisha wakazi wa
Iringa kuwa hatarini kutokana na kunywa maji yasiyo salama. Chanzo:
Hakimu Mwafongo
No comments:
Post a Comment